Friday , 26 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Ndugai amtisha Heche Tarime Vijijini
Habari za Siasa

Ndugai amtisha Heche Tarime Vijijini

Spread the love

JOB Nduga, Spika wa Bunge la Jamhuri amemtisha John Heche, Mbunge wa Tarime Vijijini kwamba, uchaguzi mkuu ujao jimbo hilo litarudi CCM mapema. Anaripoti Danson Kaijage, Dodoma … (endelea).

Ndugai amesema, kuna ufujaji mkubwa wa miradi ya serikali licha ya mbunge wake kuwa mpinzani na mpiga kelele.

Ameeleza kushangazwa na Heche kwa kushindwa kusimamia miradi ya Sh. 9 Bilioni iliyopo jimboni kwake.

“Ni lazima wabunge tujue miradi iliyo kwenye majimbo yetu,” amesema Ndugai na kuongeza;

“Sasa kama mtu kashindwa kusimamia miradi ya Sh. 9 Bilioni, mwakani atasema nini?”

Ndugai ametoa kauli hiyo leo tarehe 4 Februari 2019 bungeni Dodoma na kudai kwenye uchaguzi mkuu ujao katika jimbo hilo, wimbo utakuwa ni Sh. 9 Bilioni.

Ndugai amedai, kutokana na kushindwa kwa Heche kusimamia, ushindi kwa CCM utakuwa mapema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

error: Content is protected !!