JOB Nduga, Spika wa Bunge la Jamhuri amemtisha John Heche, Mbunge wa Tarime Vijijini kwamba, uchaguzi mkuu ujao jimbo hilo litarudi CCM mapema. Anaripoti Danson Kaijage, Dodoma … (endelea).
Ndugai amesema, kuna ufujaji mkubwa wa miradi ya serikali licha ya mbunge wake kuwa mpinzani na mpiga kelele.
Ameeleza kushangazwa na Heche kwa kushindwa kusimamia miradi ya Sh. 9 Bilioni iliyopo jimboni kwake.
“Ni lazima wabunge tujue miradi iliyo kwenye majimbo yetu,” amesema Ndugai na kuongeza;
“Sasa kama mtu kashindwa kusimamia miradi ya Sh. 9 Bilioni, mwakani atasema nini?”
Ndugai ametoa kauli hiyo leo tarehe 4 Februari 2019 bungeni Dodoma na kudai kwenye uchaguzi mkuu ujao katika jimbo hilo, wimbo utakuwa ni Sh. 9 Bilioni.
Ndugai amedai, kutokana na kushindwa kwa Heche kusimamia, ushindi kwa CCM utakuwa mapema.
Leave a comment