Thursday , 25 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa NCCR-Mageuzi yamteua Maganja kugombea urais, Z’bar wakosa
Habari za SiasaTangulizi

NCCR-Mageuzi yamteua Maganja kugombea urais, Z’bar wakosa

Spread the love

YEREMIA Kurwa Maganja ameteuliwa na Mkutano Mkuu wa chama cha upinzani nchini Tanzania cha NCCR-Mageuzi kugombea urais wa nchi hiyo katika Uchaguzi Mkuu utakaofanyika Jumatano tarehe 28 Oktoba 2020. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Mkutano huo umefanyika leo Ijumaa tarehe 7 Agosti 2020 katika ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar es Salaam na kuongozwa na James Mbatia, Mwenyekiti wa NCCR-Mageuzi.

Akitangaza matokeo ya uchaguzi, Msimamizi wa Uchaguzi, Anthony Komu amesema, wajumbe waliopiga kura walikuwa 258. Kura saba zimeharibika, kura 20 zimepugwa hapana “na kura 231 zimepigwa ndiyo sawa na asilimia 89. Kwa hiyo namtangaza Yeremia Kurwa Maganja kuwa mgombea wetu urais.”

Baada ya kutangaza matokeo hayo, Maganja aliyejiunga na NCCR-Mageuzi akitokea ACT-Wazalendo alikokuwa mwenyekiti wa chama hicho, amepewa fursa kwa mujibu wa katiba yao kumtangaza mgombea wake mwenza, Haji Ambari Khamisi.

Itakumbukwa, Khamisi alikuwa amechukua fomu ya kuwania urais wa Zanzibar lakini ndani ya mkutano huo atangaza kujitoa akisema umri umekwenda.

Awali, Komu alisema kutokana na Zanzibar kutokuwa na mgombea, Maganja ataona vyama ambavyo watashirikiana katika nafasi ya urais.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

Mpwa wa Magufuli mbaroni kwa kusambaza picha za utupu

Spread the loveJESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limewakamata...

error: Content is protected !!