Friday , 19 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Nassari ‘ashambuliwa’ kwa risasi
Habari za SiasaTangulizi

Nassari ‘ashambuliwa’ kwa risasi

Joshua Nassari, Mbunge wa Arumeru Mashariki. Picha ndogo maganda ya risasi zilizotumika kufanya katika shambulio hilo
Spread the love

MAKUMI ya watu wenye silaha, jana usiku wakiwa na bunduki na risasi za moto, walivamia nyumbani kwa mbunge wa Chadema katika jimbo la Arumeru Mashariki, Joshua Nassari, kwa lengo la kufanya mauaji, anaandika Mwandishi Wetu.

Taarifa kutoka mjini Arusha zinasema, watu hao wenye silaha, walivamia nyumbani kwa mbunge huyo, maeneo ya Usa River, majira ya saa tano na nusu usiku wa kuamkia leo Jumamosi.

Kwa mujibu wa Nassari, wakati “watu hao wasiojulikana” walivamia nyumbani kwake, muda mfupi baada ya yeye kurejea kutoka chuo cha MSTCDC (Danish), ambako alikwenda kuhudhuria mafunzo ya uongozi kwa vijana.

https://twitter.com/joshua_nassari/status/936733889405640704

“Hawa watu wameruka uzio wa nyumba yangu na kuingia ndani. Walipoingia ndani, walikutana na mbwa na wakaamua kumfyatua risasi kadhaa na kumuua,” ameeleza mbunge huyo mahiri wa Arumeru Mashariki.

Anasema, baada ya watu hao kuingia ndani na kuanza kufyatua risasi, yeye na mkewe walifanikiwa kutoroka kupitia mlango wa uani, kabla ya kuripoti tukio hilo kituo cha Polisi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari za Siasa

Mavunde aagiza Perseus kuharakisha fidia Sengerema

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameipongeza Kampuni ya Perseus kwa...

Habari za Siasa

Kigogo Chadema awanyooshea vidole vigogo serikalini kuhusu ripoti ya CAG

Spread the love  MWANACHAMA wa Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Boniface Jacob, amedai...

Habari za Siasa

Wabunge waikalia kooni TAKUKURU Bungeni

Spread the love  BAADHI ya wabunge wamelia na changamoto za utendaji wa...

Habari za SiasaTangulizi

Mpina ataka Waziri Majaliwa ajiuzulu, akosoa teuzi za mawaziri

Spread the love  MBUNGE wa Kisesa, Luhaga Mpina, amemtaka Waziri Mkuu, Kassim...

error: Content is protected !!