GODBLESS Lema, Mbunge wa Arusha Mjini, leo tarehe 14 Novemba 2019 amesema, amepewa taarifa za wito wa Jeshi la Polisi wilayani Hai, Kilimanjaro. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).
“Polisi wamevamia nyumbani kwa Mwenyekiti wa Halmshauri Hai, Helga Mchomvu, wamemkamata dereva wangu na gari yangu nyumbani kwa Helga, Nimepewa taarifa kuwa, ninatafutwa. Nimeamua kuelekea Kituo cha Polisi Hai,” Lema ameandika kwenye ukurasa wake wa twitter.
Taarifa zaidi zinaeleza kuwa, wito wa Lema kwenda polisi umetolewa na Lengai Ole Sabaya, Mkuu wa Wilaya ya Hai akidai kwenda kufanya njama za vurugu kwenye wilaya yake.
Taarifa zinaeleza, Lema alikuwa Hai kufanya vikao vya ndani vya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), na kwamba vitendo vya wanasiasa kutoka maeneo yao na kwenda maeneo mengine vimezuiwa.
Leave a comment