Friday , 19 April 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa NASA wajiondoa kwenye uchaguzi Kenya
Kimataifa

NASA wajiondoa kwenye uchaguzi Kenya

Raila Odinga, aliyekuwa mgombea wa Muungano wa NASA
Spread the love

MUUNGANO wa vyama vya Nasa umetangaza kujitoa rasmi katika uchaguzi mkuu wa Kenya uliopangwa kufanyika tarehe 26 Oktoba mwaka huu, anaandika Mwandishi Wetu.

Uamuzi wa kujiondoa katika uchaguzi huo umetangazwa leo na Raila Odinga, mgombea urais wa muu ngano wa Nasa, kwa madai kuwa uchaguzi unaotarajia kufanyika mwishoni mwa Oktoba mwaka huu si halali.

Odinga amekishutumu chama cha Jubilee na Rais Uhuru Kenyatta kwa kuanzisha mchakato wa mabadiliko ya sheria za uchaguzi katika kipindi hiki amvbacho kampeni zinaendelea na kusema kuwa hatua hiyo inalenga kukibeba chama hicho katika utangazaji wa matokeo.

Wakati hayo yakiendelea, Rais Kenyatta ameendelea na mikutano yake ya kampeni katika kaunti ya Voi ambapo amewataka Wakenya wasiyumbishwe na Odinga na chama chake na badala yake waendelee kujiandaa na uchaguzi mkuu, Oktoba 26 mwaka huu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the loveMajaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa...

Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the loveSpika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu...

Habari MchanganyikoKimataifa

Tetemeko la ardhi laua 7, lajeruhi 800 Taiwan

Spread the loveWatu wapatao saba wamefariki dunia na wengine zaidi ya 800...

error: Content is protected !!