Friday , 19 April 2024
Home Gazeti Makala & Uchambuzi Nani anaweza kuibadili CCM?
Makala & Uchambuzi

Nani anaweza kuibadili CCM?

Viongozi wa CCM wakiongoza Mkutano wa Kamati Kuu ya CCM
Spread the love

CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) kina mkondo ambao kila ajaye lazima aupite. Tusijidanganye kwamba, yupo anayeweza kubadili taswira na mfumo ndani ya CCM. Anaandika Ndoimba Nainda … (endelea).

Kinachoweza kubadilika ni sauti ya kiongozi, vitisho na ubabe-basi, lakini mengi yanayolalamikiwa huendelea kuwa yele yale.

Malilamiko yaliyoishi wakati wa utawala wa Mwalimu Julius Nyerere, Alhaj Ali Hassan Mwinyi, Benjamn Mkapa na Jakata Kikwete ndio haya haya ambayo leo watu wanayaishi.

Miongoni mwao ni msingi mibovu ya elimu, kukosekana kwa dawa, gharama za maisha kuwa juu, ubovu wa miundombinu ya maji, umeme, barabara na ufisadi.

Mwanzoni mwa utawala wa Rais Jakaya Kikwete wengi tulipata matumaini makubwa kuwa Tanzania inaingia awamu nyingine mpya ya kufagia uozo wa viongozi wanaotumia madaraka yao vibaya.

Wananasiasa Basil Pesambili Mramba na Daniel Yona wakiambata na watendaji wawili serikalini Balozi Mahalu na aliyekuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha Gray Mgonja walifikishwa mahakamani.

Si mimi pekee bali Watanzania wengi tulifanya sala maalum ili kuiombea serikali ya Rais Kikwete kuendelea na kasi hiyo.

Kuwafikisha mahakamani wengine wengi waliofanya makosa ya ufujaji wa fedha za umma, na kutumia madaraka yao kwa maslahi binafsi kulileta hisia kuwa, maisha yetu yangepumua.

Inawezekana Mungu  hakukubali ombi la kumjaza Rais Kikwete nguvu ya kupambana na uovu huo au vita hivyo na kusababisha vita hiyo kupotelea mwituni.

Tuliomba kwa dhati kabisa kwa vile yeyote anayelitakia taifa hili mema alipaswa kuunga mkono hatua hii ya serikali iliyochelewa kuwadhibiti wanasisasa na watendaji wa ngazi za juu serikalini.

Mwimbo wa maisha magumu uliimbwa kwa minajili kuwa, watendaji wabovu ndani ya serikali ya CCM ndio waliotufikisha hapo. Waliokamatwa na kupelekwa mahakamani walitoka kwa mbwembwe.

Rais Mkapa naye, aliingia kwa gia ya kubinafsisha utajiri wa Watanzania, njia za uchumi zikakabidhiwa kwa wageni. Wakawa kama wao ndio wanaoendesha uchumi, Watanzania wakabaki kuwa washangiliaji.

Wanyama, Benki, migodi, viwanda na mashirika ya umma yanakabidhiwa kwa walioitwa wawekezaji, nao hawakufanya ajizi, wakakomba kila walichoweza na wengine wameacha magofu. Hakuna kilichovunwa.

Alhaji Mwinyi alifungua milango baada ya kibano cha muda mrefu kutoka kwa Mwalimu Nyerere, hapo napo mende, popo, inzi, kunguni nao walitumia dirisha hilo hilo kuingia nchini kwa kuwa, dhamira haikuendana na uangalizi kwa manufaa ya umma.

Serikali ya sasa nayo kama ilivyokuwa zilizopita, halmashauri nako kumeoza. Trilioni 1.5 zilizotajwa kutoweka haijulikani zilinyofioweje, hakuna aliyeshitakiwa ama kusimamishwa kazi.

Mfumo wa CCM unafanya kazi, kutwa kucha kuchwa, huwezi na hutasikia CCM wakipiga kelele kuhusu kupotea kwa kiwango hichokikubwa cha fedha.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaMakala & Uchambuzi

Kanda ya Ziwa yaonyesha NMB inavyosaidia afya ya mama na mtoto

Spread the loveMafanikio inayozidi kupata Tanzania katika kupunguza vifo vya mama na...

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

‘Mwanapekee’ wa Rais Samia: Atabadili nini Arusha?

Spread the loveMAPEMA wiki hii, baadhi ya viongozi walioapishwa na Rais Samia...

Habari MchanganyikoMakala & Uchambuzi

Kipunguni waihoji serikali, ziko wapi fedha za fidia?

Spread the loveWATU wanaodai kwamba serikali ya Chama Cha Mapinduzi ni sikivu,...

Habari za SiasaMakala & UchambuziTangulizi

Askofu Bagonza: Tusichonganishwe; tusichokozane na tusikufuru

Spread the loveJOTO la chaguzi linapanda kila siku hapa nchini. Upo umuhimu...

error: Content is protected !!