Friday , 29 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Namba ya simu ya Nondo yazua taharuki
Habari za SiasaTangulizi

Namba ya simu ya Nondo yazua taharuki

Abdul Nondo, Mwenyekiti wa Mtandao wa Wanafunzi Tanzania (TSNP)
Spread the love

NAMBARI ya simu ya mkononi ya Abdul Nondo, Mwenyekiti wa Mtandao wa Wanafunzi Tanzania (TSNP), ambaye bado anashikiliwa na polisi jijini Dar es Salaam, imezua taharuki baada ya kuanza kuita bila kupokelewa huku wakati mwingine ‘aliyenayo’ akiikata. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Namba hiyo ambayo ilitoweka hewani wakati kijana huyo alipodaiwa ‘kupotea’ usiku wa kuamkia Machi 8 mwaka huu.

Kuita kwa namba hiyo bila kupokelewa huku ikikatwa inapopigiwa, kunazua sintofahamu kwani kijana huyo aliyetoweka na kupatikana akiwa Mafinga mkoani Iringa bado anashikiliwa na polisi huku mawakili, ndugu jamaa na marafiki wakizuiliwa kumuona.

Jeshi polisi Kanda Maalumu ya Dar limetoa taarifa mchana wa leo likisema “Nondo hakutekwa (alijiteka), na alitoweka jijini Dar na kuelekea Iringa kwa mpenzi wake huku akitoa taarifa zilizozua taharuki.” Hata hivyo polisi hawakumtaja anayedaiwa kuwa mpenzi wa Nondo aliyetembelewa mkoani Iringa.

Hapo awali namba ya Nondo haikuwa ikipatikana lakini leo tarehe 13 Machi, kuanzia majira ya saa tatu usiku imeripotiwa kuwa hewani na kwamba inaita na kukatwa ingawa kijana huyo yupo mikononi kwa polisi, ikiwa ni zaidi ya siku tano tangu atoweke na baadaye kushikiliwa na polisi Iringa kabla ya kusafirishwa mpaka Dar.

Haijajulikana mara moja ikiwa anayetumia namba hiyo ni Nondo mwenyewe, maofisa wa polisi wanaofanya upelelezi au mtu mwingine.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

error: Content is protected !!