Thursday , 25 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Namaingo wazindua mradi mpya Msolwa
Habari Mchanganyiko

Namaingo wazindua mradi mpya Msolwa

Biubwa Ibrahimu, Mkurugenzi wa Namaingo
Spread the love

JUHUDI za Taasisi ya Namaingo Business Agents (NBA), imezindua mradi Shamba Mji Msolwa wilayani Mkuranga, Pwani ikiwa ni mwendelezo wa kuinua uchumi wa nchi kupitia kilimo. Anaripoti Faki Sosi … (endelea).

Mradi wa Shamba Mji utakuwa na hekari 7,000 ambapo utahusisha mashamba na makazi pamoja na huduma za kijamii ikiwa pamoja na soko la kuuza mazao yatakayotokana na mazao ya shamba hilo.

Biubwa Ibrahimu, Mkurugenzi wa Namaingo amesema uzinduzi mashamba hayo yatakuwa kichecheo kikubwa cha kunyanyua uchumi wa wakulima, wakazi wanaozunguka maeneo ya mashamba na nchi kwa ujumla.

Amesema kupitia mradi huo wakulima watapata fulsa ya kupata ushauri wa kupanda mazao kwa ubora ikiwa pamoja na kugeuza kutoka kilimo cha chakula na kulima kilimo cha biashara.

Diwani wa Kata ya Mbezi, Rashid Selungwi, amesema kuwa wananchi wa eneo hilo wamefurahia ujio wa mradi huo utakaowaletea maendeleo makubwa kwani hiyo ni moja ya fulsa kwa wakazi wa Msolwa.

Mwakilishi wa Wazee wa kijiji cha Msolwa, Ali Kitasa ameubariki mradi huo na kuwaombea dua walulima watakaojishughulisha na mradi huo kwani anaamini kuwa mafanikio yao yatawagusa wakazi wa eneo hilo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

THRDC yaongeza mkataba wa ushirikiano na ABA

Spread the love  MTANDAO wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC),...

Habari Mchanganyiko

Rufaa ya Equity Benki, State Oil yakwama

Spread the loveMAHAKAMA ya Rufani, jijini Dar es Salaam, imeshindwa kuendelea na...

error: Content is protected !!