Friday , 29 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Naibu Meya wa Dar atimkia CCM
Habari za Siasa

Naibu Meya wa Dar atimkia CCM

Mussa Kafana, Aliyekuwa Naibu Meya Dar es Salaam
Spread the love

ALIYEKUWA Naibu Meya wa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam, Mussa Kafana amejiuzulu uanachama wa CUF na kuomba kupokelewa ndani ya CCM. Anaripoti Regina Kelvin … (endelea).

Kafana ambaye pia alikuwa diwani wa kata ya Kiwalani ametangaza kujivua uanachama wa CUF pamoja na kujiuzulu udiwani na unaibu meya wa jiji la Dar es Salaam leo tarehe 18 Agosti, 2018 wakati akizungumza na wanahabari jijini hapa.

Akielezea sababu za kujiuzulu, Kafana amesema mgogoro unaoendelea katika chama hicho unamyima fursa ya kisiasa na hivyo amemaua kuhamia katika chama kisicho na migogoro.

“CUF ina pande mbili zinavutana na mngogoro huu hauwezi kuisha leo wala kesho kwa sababu wanachobishana na kuvutana ni watu wakubwa kwenye chama. Sijaongea na kiongozi yoyote wa CCM na sijajiunga na chama chochote cha siasa ila kama viongozi wa chama hicho wananisikia na watanipokea nitashukuru naomba nipokelewe,” amesema Kafana.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

error: Content is protected !!