Thursday , 28 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Nafasi ya Gambo Arusha yajazwa
Habari za Siasa

Nafasi ya Gambo Arusha yajazwa

Mrisho Gambo, Mbunge wa Arusha Mjini (CCM)
Spread the love

MKUU wa Mkoa wa Arusha sasa ni Idd Kimanta, ambaye awali alikuwa Mkuu wa Wilaya ya Monduli jijini Arusha. Anaripoti Faki Sosi, Dar es Salaam…(endelea).

Uteuzi huo umefanywa leo tarehe 21 Juni 2020 na Rais John Mafufuli.

Kabla ya uteuzi wa Kimanta le tarehe 21 Juni 2020, mkoa huo ulikuwa ukiongozwa na Mrisho Gambo ambaye ametumbuliwa Ijumaa tarehe 19 Juni 2020.

Katika taarifa yake, Mkurugeni wa Mawasiliano Ikulu, jijini Dar es Salaam Gerson Msigwa imeeleza, nafasi ya Kimanta (Monduli) sasa itashikiliwa na Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP), Edward Jotham Balele. Balale alikuwa Wizara ya Mambo ya Ndani Nchi.

Pia Rais Maguduli amemteua Bakari Msulwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Morogoro, baada ya Rigina Chonjo, aliyekuwa akiongoza wilaya hiyo kustaafu.

Msulwa alikuwa ofisa mwandamizi na mtangazaji wa Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC).

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

Habari za SiasaTangulizi

CAG aibua madudu halmashauri 10, TANESCO na MSD

Spread the loveRIPOTI ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali...

Habari za Siasa

Alichokisema Rais Samia baada ya kupokea ripoti ya CAG, TAKUKURU

Spread the loveRAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Serikali yake itafanyia kazi...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga kuongoza usambazaji wa mitungi ya gesi 10,000 ya Taifa Gas

Spread the loveNaibu Waziri wa Nishati, Judith Kapinga ameahidi kuongoza kwa ufanisi...

error: Content is protected !!