MKUU wa Mkoa wa Arusha sasa ni Idd Kimanta, ambaye awali alikuwa Mkuu wa Wilaya ya Monduli jijini Arusha. Anaripoti Faki Sosi, Dar es Salaam…(endelea).
Uteuzi huo umefanywa leo tarehe 21 Juni 2020 na Rais John Mafufuli.
Kabla ya uteuzi wa Kimanta le tarehe 21 Juni 2020, mkoa huo ulikuwa ukiongozwa na Mrisho Gambo ambaye ametumbuliwa Ijumaa tarehe 19 Juni 2020.
Katika taarifa yake, Mkurugeni wa Mawasiliano Ikulu, jijini Dar es Salaam Gerson Msigwa imeeleza, nafasi ya Kimanta (Monduli) sasa itashikiliwa na Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP), Edward Jotham Balele. Balale alikuwa Wizara ya Mambo ya Ndani Nchi.
Pia Rais Maguduli amemteua Bakari Msulwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Morogoro, baada ya Rigina Chonjo, aliyekuwa akiongoza wilaya hiyo kustaafu.
Msulwa alikuwa ofisa mwandamizi na mtangazaji wa Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC).
Leave a comment