Friday , 19 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Mzungu kortini kwa kukutwa na fuvu la Nyumbu.
Habari Mchanganyiko

Mzungu kortini kwa kukutwa na fuvu la Nyumbu.

Nyundo ya Hakimu
Spread the love

RAIA wa  Denmark Ricki Thomson (49), amepandishwa kizimbani katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam  kwa kosa ka kukutwa fuvu la Nyumbu., Anaandika Faki Sosi.

Mtuhumiwa huyo amekutwa na fuvu hilo bila kibari cha Mkurugenzi wa wanyama pori nchini.

Mbele ya Hakimu Mfawidhi wa Mahakama hiyo,  Cyprian Mkeha, Wakili wa Serikali Kishenyi Mutalemwa akiwa amedai  kuwa tukio hilo lilitokea Oktoba 9, mwaka huu katika Uwanja Ndege wa Kimataifa Julius Nyerere bila kuwa na kibali.

“Ulikamatwa na fuvu hilo bila kuwa na kibali kutoka kwa Mkurugenzi wa wanyama pori nchini,” amedai Kishenyi.

Baada ya kusomewa mashtaka hayo mtuhumiwa amekana na upande wa Jamhuri umedai kukamilisha upelelezi
Kesi hiyo imeahirishwa hadi Oktoba 16, mwaka huu itakapokuja kutajwa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB Pesa Akaunti yawavutia wakaguzi wa ndani Afrika

Spread the loveUbunifu wa bidhaa bora wa Benki ya NMB pamoja na...

Habari Mchanganyiko

Carbon First, Ruangwa wasaini makubaliano ya biashara ya hewa ukaa

Spread the love  KAMPUNI ya Carbon First Tanzania Limited na Halmashauri ya...

Habari Mchanganyiko

CBE yawakumbuka wenye mahitaji maalum Jangwani

Spread the loveCHUO cha Elimu ya Biashara (CBE), kimetoa msaada mbalimbali na...

Habari Mchanganyiko

Mume auwa mke kwa kumchoma visu, ajisalimisha Polisi

Spread the loveJACKSON Kalamji (49), anashikiliwa na Jeshi la Polisi jijini Mwanza,...

error: Content is protected !!