MFALME wa maigizo ya uchekeshaji nchini, Amri Athuman anayefahamika kama ‘Mzee Majuto’ amelazwa chumba cha wagonjwa mahtuti (ICU) kwenye hospitali ya Taifa Muhimbili. Anaripoti Regina Kelvin … (endelea).
Taarifa hizo zimethibitishwa na Afisa Habari wa Chama cha Waigizaji, Masoud Kaftany ambaye amesema kuwa, Mzee Majuto kwa sasa anafanyiwa vipimo ili kubaini ugonjwa unaomsumbua.
Naye Mkurugenzi wa Mawasiliano Hospitali ya Taifa ya Muhimbilli, Aminiel Aligaesha amethibitisha uwepo wa Mzee majuto hospitalini hapo.
Aligaesha amesema Mzee Majuto yuko kwenye chumba cha wagonjwa mahututi hospitalini hapo, baada ya kuletwa siku ya Jumanne majira ya saa kumi na mbili jioni.
Leave a comment