Friday , 29 March 2024
Home Kitengo Michezo Mzee Chumo atetea vipaji vipya
Michezo

Mzee Chumo atetea vipaji vipya

Spread the love

MSANII nyota wa filamu nchini Tanzania, Jafari Makatu maarufu kwa jina la Mzee Chumo, amewataka waandaaji wa filamu kuacha kuzima vipaji vichanga vya wasanii kwa kuendekeza ubaguzi. Anaripoti Hamis Mguta…(endelea).

Akizungumza na MwanaHALISI Online nyota huyo anayewika kwenye thamthilia ya Huba amesema kuwa, kitendo hicho kimekuwa kikiua vipaji vya wasanii wachanga kutokana na kutopata nafasi ya kuonesha vipaji vyao.

“Watu wanafanya hivyo lakini sio sahihi kwasababu unawanyima haki wasanii wanaokuja. Hawa wapya wana wana vionjo vya kipekee na wana hamu ya kuonekana na kuweka majina yao kwenye kiwango cha juu, hivyo wanakuja na mtindo mwingine ambao unamfanya mtazamaji apende,” amesema.

Mzee Chumo amesema kuwa, makosa mengi yanatokana na waandishi na waongozaji wa filamu kutokana na watu kuwa waongozaji hata kama wakiwa hawafahamu maana halisi ya uongozaji.

Mwigizaji huyu aliwahi kufanya kazi hizo na marehemu Sharo Milionea, Yusuph Mlela pamoja na Jokate Mwegelo ambaye kwasasa ni Mkuu wa Wilaya ya Kisarawe.

“Mtu akicheza filamu tatu tu anakuja na yeye anakuwa muongozaji (Director), lakini hajui majukumu ya muongozaji na wala hajui muongozaji ni mtu wa aina gani,” amesema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Makala & UchambuziMichezo

TFF kuamua hatima ya Amrouche

Spread the loveHATIMA ya Kocha Mkuu wa Taifa Stars, Adel Amrouche kuendelea...

Habari za SiasaMichezo

Matinyi: Dk. Ndumbaro alifanya utani ukaguzi mechi za Yanga, Simba

Spread the loveMsemaji Mkuu wa Serikali, Mobhare Matinyi amesema kauli iliyotolewa na...

Michezo

Gethsemane Group Kinondoni (GGK) waachia video ya Bwana Wastahili

Spread the loveWAIMBAJI maarufu nchini kutoka Gethsemane Group Kinondoni (GGK)SDA wameachia video...

BiasharaMichezo

Gamondi kocha bora mwezi Februari, NBC yamjaza manoti

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambae ni mdhamini Mkuu...

error: Content is protected !!