Tuesday , 19 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Waitara ajikomba kwa Rais Magufuli
Habari za Siasa

Waitara ajikomba kwa Rais Magufuli

Mwita Waitara, aliyekuwa Naibu Waziri wa Muungano na Mazingira
Spread the love

MWITA Waitara, Naibu Waziri wa TAMISEMI na Mbunge wa Jimbo la Ukonga, jijini Dar es Salaam amejikomba kwa Rais John Magufuli. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam…(endelea).

Amemwambia Rais Magufuli kwamba, atavuna kura nyingi za urais kwa kuwa, nafasi aliyompa ya uwanaibu waziri wa TAMISEMI, umemuezesha kujua hilo kutokana na kutembea sehemu mbalimbali.

Ametoa kauli hiyo leo tarehe 23 Januari 2020, katika hafla ya makabidhiano ya nyumba za maofisa na askari wa jeshi la magereza, zilizoko jimboni mwake (Ukonga), jijini Dar es Salaam.

“…mwaka huu utavunja rekodi ambayo haijawahi kupatikana kwenye taifa hili,” ameeleza Mwita na kwamba, alikopita uchaguzi wa rais umekwisha.

“Kote nilikopita wanasema, uchaguzi wa rais umeisha na utaweka historia, mara zote tukifanya uchaguzi huwa kura za urais awamu ya kwanza zinakuwa nyingi, inayofuata zinakuwa chache, naomba nikuhakikishie mwaka huu itakuwa vice versa (kinyume chake).” amesema Mwita.

Mwita amedai, Rais Magufuli atavunja historia katika matokeo ya uchaguzi wa mwaka huu, kwa kuwa uongozi wake umeacha alama kwa Watanzania wengi.

“Kwa nafasi uliyonipa ya naibu waziri, nimezunguka nchi hii, Bwana Yesu anasema, wasipoamini watu wake waamini kupitia matendo ya watu wake. Mhehsimwia rais Watanzania, wataamini kupitia matendo yako na ni kiongozi ambaye unaacha alama,” amesema Mwita.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari za Siasa

Zanzibar mbioni kuanza uchimbaji mafuta na gesi baharini

Spread the loveSERIKALI ya Zanzibar, imekamilisha mchakato wa uchimbaji wa mafuta na...

Habari za Siasa

Wizara ya afya yataja mafanikio 10 miaka mitatu Samia madarakani

Spread the loveWIZARA ya Afya imetaja mafanikio 10 iliyoyapata ndani ya miaka...

Habari za Siasa

Mbozi walilia kuwa manispaa, majimbo 3

Spread the loveHALMASHAURI ya wilaya ya Mbozi mkoani Songwe imeeleza dhamira yake...

Habari za Siasa

Wabunge waitaka TPDC kuongeza kasi ya kuunganisha wateja gesi asilia

Spread the love  KAMATI ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini...

error: Content is protected !!