Thursday , 28 March 2024
Habari za SiasaTangulizi

Mwingine apotea​

Mkurugenzi wa Idara ya Haki na Wajibu wa Wanafunzi Tanzania, Abdul Nondo
Spread the love

ADUL Nondo, mwanafunzi wa mwaka wa tatu katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), ambaye alikuwa mstari wa mbele kupinga kitendo cha jeshi la Polisi kumpiga risasi, Akwiline Akwelina, amepotea katika mazingira ya kutatanisha. Anaripoti Saed Kubenea … (endelea).

Taarifa kutoka kwa watu waliokaribu na Nondo zinasema, kabla ya “kupotea” hewani, mwanafunzi huyo alijitoa kwenye makundi yote ya mtandao wa Whatsapp aliyokuwa amejiunga.

Nondo ambaye ni mwenyekiti wa TSNP, amekuwa mstari wa mbele kushinikiza serikali kufanya uchunguzi wa mauaji ya Akwiline.

Akwiline aliuawa kwa kupigwa risasi na jeshi la Polisi, tarehe 6 Februari mwaka huu, kwenye maeneo ya Mkwajuni, Kinondoni, jijini Dar es Salaam, akiwa ndani ya basi ya daladala.

Akwiline alikuwa akitokea maeneo ya Mabibo kwenda Bagamoyo kwa mafunzo ya vitendo.

Habari zinasema, taarifa rasmi kwa umma zitatolewa kwa waandishi wa habari saa majira ya 9:30 alasiri kwenye ukumbi wa Kituo cha Sheria na Haki Za Binadamu LHRC.

Katika siku za karibuni, kumeibuka kundi kubwa la vitendo vya utekaji, utesaji na mauaji nchini.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifa

Mwanaye rais jela miaka miaka 6 kwa dawa za kulevya

Spread the loveMwanawe rais wa zamani wa Guinea-Bissau amehukumiwa kifungo cha miaka...

Habari za SiasaTangulizi

Mapya yaibuka wamasai waliohamishwa Ngorongoro kwenda Msomera

Spread the loveMAPYA yameibuka kuhusu zoezi la Serikali kuwahamisha kwa hiari wamasai...

Habari MchanganyikoTangulizi

Baba aomba msaada kuzika miili ya familia yake iliyofunga bila kula kuonana na Mungu

Spread the loveWAKATI Mamlaka nchini Kenya, ikiendelea kukabidhi miili ya watu waliofariki...

Habari za Siasa

Rais Samia ampongeza mpinzani aliyeshinda urais Senegal

Spread the loveRAIS wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu Hassan, amempongeza mwanasiasa wa...

error: Content is protected !!