Friday , 19 April 2024
Home Kitengo Michezo Mwina Kaduguda aitaka tena Simba
Michezo

Mwina Kaduguda aitaka tena Simba

Spread the love

BAADA kukamilika kwa zoezi la uchukuaji fomu kuwania uongozi ndani ya klabu ya Simba, kamati ya uchaguzi ndani ya klabu hiyo imetoa orodha ya majina 21 ya wanachama waliojitokeza kuwania nafasi za ujumbe wa bodi ya Ukurugenzi ndani ya klabu hiyo. Anaripoti Kelvin Mwaipungu … (endelea).

Katika nafasi ya Mwenyekiti waliojitokeza ni watu wawili Swedi Khamisi na Mtemi Rmadhani, kwenye nafasi ya wajumbe kwa upande wa wanawake waliochukua fomu ni Jasmine Soudy na Asha Baraka, huku kwenye nafasi ya ujumbe waliojitokeza ni watu 17.

Waliochukua fomu za ujumbe ni Hussen Mlinga, Iddi Kajuna, Said Tuli, Zawadi Kadunda, Mohamed Wandi, Selemani Said, Abdalaah Mgomba, Christopher Mwansasu, Alfred Elia, Mwina Kaduguda, Juma Pinto, Ally Suru, Hamisi Mkoma, Abubakari Zebo, Omari Mazola, Patrick Rweyemamu na Seleman Seleman.

Kamati hiyo ya usajili pia imesema zoezi la urudishaji fomu litaanza siku ya Jumanne tarehe 11 septemba 2018 hadi Jumamosi 15 Septemba mwaka huu huku wakiambatanisha pamoja na nakala za vyeti vyao vilivyothibitishwa na vyuo husika.

Uchaguzi wa klabu hiyo unatarajiwa kufanyika Novemba 3, mwaka huu baada ya kubadilisha mfumo wa uendeshaji ndani ya klabu hiyo na kwenda kwenye mfumo wa kibiashara ambao unaoenekana kuwa na manufaa makubwa kwa klabu kiujumla.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Piga pesa na mechi za EUROPA leo hii

Spread the love Hatimaye Alhamisi ya EUROPA imefika ambapo leo hii mechi...

Michezo

Leo ni leo nani kutinga nusu fainali UEFA?

Spread the love HATIMAYE Jumanne ya UEFA imefika ambapo leo hii michezo...

Michezo

Anza Jumatatu yako na Meridianbet

Spread the love  IKIWA ni siku nyingine mpya kabisa ya Jumatatu baadhi...

Habari MchanganyikoMichezo

NBC, Yanga wazindua kadi  za kimataifa za uanachama

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) kwa kushirikiana na Klabu...

error: Content is protected !!