MWILI wa Dk. Reginald Mengi, aliyekuwa mwenyekiti wa kampuni zilizo chini ya IPP Group, tayari umewasili kwenye Uwanja wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA). Anaripoti Hamisi Mguta, Kilimanjaro … (endelea).
Viongozi mbalimbali wa serikali, mila, ndugu, jamaa na marafiki mkoani humo, wamejitokeza kuulaki mwili wa Dk. Mengi ambaye ulibebwa na Shirika la Ndege la Precision asubuhi ya leo tarehe 8 Mei 2019 na kutua KIA.
Dk. Mengi anatarajiwa kuzikwa kesho tarehe 9 Mei 2019 kijijini kwake Machame, Moshi baada ya shughuli ya ibada na taratibu zingine kufanyika.
Mfanyabiashara huyo (Dk. Mengi), alifariki dunia usiku wa kuamkia tarehe 2 Mei 2019 Dubai, Falme za Kiarabu.
Leave a comment