Thursday , 25 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Mwili wa Dk. Mengi watua Kilimanjaro
Habari MchanganyikoTangulizi

Mwili wa Dk. Mengi watua Kilimanjaro

Spread the love

MWILI wa Dk. Reginald Mengi, aliyekuwa mwenyekiti wa kampuni zilizo chini ya IPP Group, tayari umewasili kwenye Uwanja wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA). Anaripoti Hamisi Mguta, Kilimanjaro … (endelea).

Viongozi mbalimbali wa serikali, mila, ndugu, jamaa na marafiki mkoani humo, wamejitokeza kuulaki mwili wa Dk. Mengi ambaye ulibebwa na Shirika la Ndege la Precision asubuhi ya leo tarehe 8 Mei 2019 na kutua KIA.

Dk. Mengi anatarajiwa kuzikwa kesho tarehe 9 Mei 2019 kijijini kwake Machame, Moshi baada ya shughuli ya ibada na taratibu zingine kufanyika.

Mfanyabiashara huyo (Dk. Mengi), alifariki dunia usiku wa kuamkia tarehe 2 Mei 2019 Dubai, Falme za Kiarabu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

error: Content is protected !!