Thursday , 28 March 2024
Home Habari Mchanganyiko Mwijage ‘aibuka’ na parachichi bungeni
Habari Mchanganyiko

Mwijage ‘aibuka’ na parachichi bungeni

Kilimo cha parachichi
Spread the love

CHARLES Mwijage, waziri wa zamani wa Viwanda na Mbunge wa Kaskazini (CCM), ameitaka serikali kueleza mpango wake katika kuwezesha wakulima wa zao la parachichi mkoani Kagera. Anaripoti Danson Kaijage, Dodoma … (endelea).

Amehoji, kwa kuwa zao hilo lina mahitaji ya kitaalam katika kulima mpaka kuvuna, kwanini serikali isiwapatie mafunzo maalum wataalam angalau wawili katika kila Wilaya za Mkoa wa Kagera ili waweze kuwaongoza wananchi wanaolima zao hilo?.

Leo tarehe 14 Aprili 2020, Wizara ya Kilimo imejibu swali hilo kwamba, zao la parachichi ni moja kati ya mazao ya asili ya matunda yanayozalishwa Kagera.

Imeeleza, wakulima wengi wamehamasika kuzalisha zao hilo kutokana na kuwepo kwa soko la kimataifa la parachichi hususan aina za HASS na FUERTE.

“Katika kuhakikisha kuwa wakulima wa parachichi mkoani Kagera wanapata miche bora, Wizara ya Kilimo kupitia Kituo cha Utafiti wa Kilimo cha TARI- Maruku, imeendelea kuzalisha na kusambaza miche bora ya parachichi katika Halmashauri za Mkoa wa Kagera.

“Katika msimu wa 2018/19, Kituo cha Utafiti Maruku kilizalisha na kusambaza miche 4,000 ya zao la parachichi kwa wakulima wa Halmashauri za Karagwe, Misenyi na Muleba” imeeleza wizara.

Aidha, imeeleza katika msimu wa 2019/20, kituo cha TARI Maruku kitazalisha miche ya parachichi 10,000 itakayosambazwa na kuuzwa kwa wakulima wa Kagera kwa bei nafuu.

“Wizara kwa kushirikiana na Halmashauri ya Wilaya za Mkoa wa Kagera, imeendelea kutoa elimu kuhusu uzalishaji wa miche bora ya zao la parachichi kupitia maonesho ya Nanenane msimu wa mwaka 2019/2020, na maafisa ugani wanne (4) kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Misenyi, walipatiwa elimu ya uzalishaji wa miche bora ya parachichi.

“Vilevile, wakulima zaidi ya 300 walipatiwa elimu ya uzalishaji wa zao la parachichi kupitia maonesho ya wiki ya uwekezaji mkoani Kagera yaliyofanyika Agosti, 2019.

“Wizara kupitia TARI Maruku kwa kushirikiana na Halmashauri za Wilaya za Mkoa wa Kagera zimeandaa mpango wa mafunzo kwa wataalam wa kilimo katika Halmashauri za Mkoa wa Kagera kuhusu mbinu bora za uzalishaji wa zao la parachichi ili waweze kutoa elimu hiyo kwa wakulima wa zao la parachichi,” wizara imeeleza.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Mtandao watetezi wa haki za mazingira Tanzania waundwa

Spread the loveMTANDAO wa watetezi wa haki za mazingira nchini Tanzania, umeundwa...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga kuongoza usambazaji wa mitungi ya gesi 10,000 ya Taifa Gas

Spread the loveNaibu Waziri wa Nishati, Judith Kapinga ameahidi kuongoza kwa ufanisi...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wafanyabiashara, wawekezaji China waridhia kuwekeza bil. 800 katika sekta 5 nchini

Spread the loveUJUMBE wa wafanyabiashara na wawekezaji wakubwa kutoka Jimbo la Changzhou...

Habari Mchanganyiko

Bil. 4.42 kumaliza uhaba maji kata 2 Musoma Vijijini

Spread the loveWANANCHI wa kata za Busambara na Kiriba, Jimbo la Musoma...

error: Content is protected !!