Tuesday , 23 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mwigulu Nchemba atupwa nje Baraza la Mawaziri
Habari za SiasaTangulizi

Mwigulu Nchemba atupwa nje Baraza la Mawaziri

Spread the love

RAIS John Magufuli amefanya mabadiliko madogo ya baraza la mawaziri na kumteua Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), Kangi Lugola kuwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, nafasi ambayo awali ilikuwa ikishikiliwa na Dk Mwigulu Nchemba. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi John Kijazi amesema mbali na kufanya mabadiliko ya baraza hilo, rais ameteua makatibu wakuu, naibu makatibu wakuu, mkurugenzi wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), makamishna wa tume hiyo na balozi mmoja. 

Balozi Kijazi amesema mbali na uteuzi wa Kangi, Rais Magufuli amemteua mbunge wa Singida Mjini, Mussa Sima kuwa Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira).

Pia, amewabadilisha wizara Profesa Makame Mbarawa ambaye alikuwa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano na sasa amekuwa Waziri wa Maji na Umwagiliaji.

Aliyekuwa Waziri wa Maji na Umwagiliaji, mhandisi Isaack Kamwelwe ameteuliwa kuwa Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano.

Balozi Kijazi amesema kutokana na umuhimu na uzito wa majukumu katika sekta ya kilimo, Rais Magufuli ameongeza naibu waziri katika Wizara ya Kilimo kwa kumteua mbunge wa Morogoro Kusini Mashariki, Omary Mgumba. Kwa uteuzi huo wizara hiyo sasa itakuwa na naibu mawaziri wawili; Mgumba na Dk Mary Mwanjelwa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Rais Samia aridhishwa utendaji mabalozi, awapa neno

Spread the loveRais wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu Hassan amewapongeza mabalozi  wanaowakilisha ...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

NMB yadhamini Mkutano Mkuu ALAT, kufunguliwa na Samia

Spread the loveBENKI ya NMB, imekabidhi hundi yenye thamani ya Sh. 120...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mipango na uwekezaji kutumia bilioni 121.3, mradi wa Bagamoyo wapewa kipaumbele

Spread the loveWIZARA ya Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji, imeliomba Bunge...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mbunge ataka kasi uzalishaji walimu ipunguzwe akidai hakuna ajira

Spread the loveMBUNGE wa Mlalo (CCM), Rashid Shangazi, ameishauri Serikali ipunguze kasi...

error: Content is protected !!