Friday , 19 April 2024
Home Gazeti Makala & Uchambuzi Mwenyekiti wa Tume Kenya amtuliza Raila Odinga
Makala & Uchambuzi

Mwenyekiti wa Tume Kenya amtuliza Raila Odinga

Wafula Chebukata, Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi na Mipaka ya Kenya (IEBC)
Spread the love

WAFULA Chebukati, Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi na Mipaka Nchini Kenya (IBEC), ameahidi kushughulikia malalamiko yaliyotolewa na mgombea urais kupitia Muungano wa NASA, Raila Odinga, juu ya kuwepo kwa madai ya udanganyifu kwenye uhesabuji wa kura, anaandika Victoria Chance.

Amesema fomu 34A na 34B ziko tayari na wameandaa dawati la mawakala wakuu kwaajili ya kuchunguza fomu 34A na 34B, “…tutajua kama haya malalamiko ni ya kweli na kama siyo ya ukweli hatutayazingatia.”

Chebukati amewataka Wakenya kuvuta subira na matokeo ya mwisho bado hayajatolewa na kwamba yatatolewa baada ya siku tano kuanzia leo.

Leo mapema asubuhi, Odinga aliitaka Tume hiyo kuhakikisha inatumia fomu namba 34 A kama sheria inavyotaka, wakati wa kujumlisha na kutangaza matokeo ya uchaguzi mkuu nchini Kenya.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaMakala & Uchambuzi

Kanda ya Ziwa yaonyesha NMB inavyosaidia afya ya mama na mtoto

Spread the loveMafanikio inayozidi kupata Tanzania katika kupunguza vifo vya mama na...

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

‘Mwanapekee’ wa Rais Samia: Atabadili nini Arusha?

Spread the loveMAPEMA wiki hii, baadhi ya viongozi walioapishwa na Rais Samia...

Habari MchanganyikoMakala & Uchambuzi

Kipunguni waihoji serikali, ziko wapi fedha za fidia?

Spread the loveWATU wanaodai kwamba serikali ya Chama Cha Mapinduzi ni sikivu,...

Habari za SiasaMakala & UchambuziTangulizi

Askofu Bagonza: Tusichonganishwe; tusichokozane na tusikufuru

Spread the loveJOTO la chaguzi linapanda kila siku hapa nchini. Upo umuhimu...

error: Content is protected !!