Saturday , 20 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Skauti sasa kutua Vyuo Vikuu
Habari za Siasa

Skauti sasa kutua Vyuo Vikuu

Mwantumu Mahiza, Skauti Mkuu wa Chama cha Maskauti Tanzania
Spread the love

BAADA ya kuteuliwa na kuapishwa kuwa Skauti Mkuu wa Chama cha Maskauti Tanzania, Mwantumu Mahiza ameahidi kuieneza skauti katika vyuo vya kati na vyuo vikuu. Anaripoti Regina Kelvin … (endelea).

Mahiza ameyaahidi hayo leo tarehe 3 Oktoba 2018 ikulu jijini Dar es Salaam, ambapo alimhakikishia Rais John Magufuli kwamba atautumia vyema wadhifa huo katika kujenga maadili ya vijana wa kitanzania.

Mahiza ameeleza kuwa, kwa miaka mingi skauti ilienea katika shule za msingi na sekondari na kwamba ni wakati husika kwa taasisi hiyo ya kujenga maadili ya vijana wa Tanzania kuenea katika vyuo vyote hapa nchini.

“Nakushukuru kwa kuniteua kulea vijana wa Tanzania kupitia skauti, wajibu wangu ni mambo mawili, kuhakikisha skauti inaenea katika vyuo vya kati na vyuo vikuu kwa sababu miaka mingi ilienea shule za msingi na sekondari,” amesema Mahiza.

Katika hatua nyingine, Mahiza aliahidi kufanikisha ujenzi wa kambi ya kimataifa ya Skauti jijini Dodoma.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari za Siasa

Mavunde aagiza Perseus kuharakisha fidia Sengerema

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameipongeza Kampuni ya Perseus kwa...

Habari za Siasa

Kigogo Chadema awanyooshea vidole vigogo serikalini kuhusu ripoti ya CAG

Spread the love  MWANACHAMA wa Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Boniface Jacob, amedai...

Habari za Siasa

Wabunge waikalia kooni TAKUKURU Bungeni

Spread the love  BAADHI ya wabunge wamelia na changamoto za utendaji wa...

Habari za SiasaTangulizi

Mpina ataka Waziri Majaliwa ajiuzulu, akosoa teuzi za mawaziri

Spread the love  MBUNGE wa Kisesa, Luhaga Mpina, amemtaka Waziri Mkuu, Kassim...

error: Content is protected !!