Tuesday , 19 March 2024
Home Kitengo Michezo Mwanjali anyakuwa Tuzo ya mchezaji bora wa mwezi
Michezo

Mwanjali anyakuwa Tuzo ya mchezaji bora wa mwezi

Method Mwanjali, Beki raia wa Zimbabwe anayekipiga ndani ya klabu ya Simba
Spread the love

BEKI raia wa Zimbabwe anayekipiga ndani ya klabu ya Simba, Method Mwanjali amechaguliwa kuwa mchezaji bora ndani ya klabu hiyo katika mwezi Disemba, 2016 kutokana msaada mkubwa alioutoa ndani ya kikosi hicho katika michezo iliyopita, anaandika Kelvin Mwaipungu.

Mwanjali ambaye ndio msimu wake wa kwanza kuitumikia klabu ya Simba , amekuwa na msaada mkubwa katika idara ya ulinzi, na kusababisha timu hiyo kuruhusu mabao 6 katika michezo 18 ya ligi waliocheza na kufanya timu iliyoruhusu mabao machache katika ligi kuu.

Utaratibu wa kutoa zawadi ya mchezaji bora ndani ya klabu hiyo ulianza mwaka 2015 mwezi Septemba, kwa lengo la kuwapa motisha wachezaji ili waweze kujituma zaidi na kuwapa zawadi ya shilingi laki tano.

Klabu hiyo ambayo inaongoza ligi kwa sasa, muda mchache ujao watashuka dimbani katikia mchezo wa ligi kuu dhidi ya Mtibwa Sugar utakaopigwa katika uwanja wa Jamhuri uliopo Morogoro.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Gethsemane Group Kinondoni (GGK) waachia video ya Bwana Wastahili

Spread the loveWAIMBAJI maarufu nchini kutoka Gethsemane Group Kinondoni (GGK)SDA wameachia video...

BiasharaMichezo

Gamondi kocha bora mwezi Februari, NBC yamjaza manoti

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambae ni mdhamini Mkuu...

Michezo

Tusua kijanja na mechi za Europa leo

Spread the love  Alhamisi ya leo EUROPA inaendelea ambapo ni mechi za...

Michezo

Hapa Diego Simeone, pale Simeone Inzaghi kivumbi cha Ligi ya Mabingwa Ulaya

Spread the love LIGI ya Mabingwa ulaya itaendelea usiku wa leo ambapoitakwenda...

error: Content is protected !!