Friday , 19 April 2024
Home Kitengo Michezo Mwanjali anyakuwa Tuzo ya mchezaji bora wa mwezi
Michezo

Mwanjali anyakuwa Tuzo ya mchezaji bora wa mwezi

Method Mwanjali, Beki raia wa Zimbabwe anayekipiga ndani ya klabu ya Simba
Spread the love

BEKI raia wa Zimbabwe anayekipiga ndani ya klabu ya Simba, Method Mwanjali amechaguliwa kuwa mchezaji bora ndani ya klabu hiyo katika mwezi Disemba, 2016 kutokana msaada mkubwa alioutoa ndani ya kikosi hicho katika michezo iliyopita, anaandika Kelvin Mwaipungu.

Mwanjali ambaye ndio msimu wake wa kwanza kuitumikia klabu ya Simba , amekuwa na msaada mkubwa katika idara ya ulinzi, na kusababisha timu hiyo kuruhusu mabao 6 katika michezo 18 ya ligi waliocheza na kufanya timu iliyoruhusu mabao machache katika ligi kuu.

Utaratibu wa kutoa zawadi ya mchezaji bora ndani ya klabu hiyo ulianza mwaka 2015 mwezi Septemba, kwa lengo la kuwapa motisha wachezaji ili waweze kujituma zaidi na kuwapa zawadi ya shilingi laki tano.

Klabu hiyo ambayo inaongoza ligi kwa sasa, muda mchache ujao watashuka dimbani katikia mchezo wa ligi kuu dhidi ya Mtibwa Sugar utakaopigwa katika uwanja wa Jamhuri uliopo Morogoro.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Tusua mkwanja na mechi za Ijumaa leo

Spread the love  LEO hii mechi zinaendelea kote na wewe kama unataka...

Michezo

Piga pesa na mechi za EUROPA leo hii

Spread the love Hatimaye Alhamisi ya EUROPA imefika ambapo leo hii mechi...

Michezo

Leo ni leo nani kutinga nusu fainali UEFA?

Spread the love HATIMAYE Jumanne ya UEFA imefika ambapo leo hii michezo...

Michezo

Anza Jumatatu yako na Meridianbet

Spread the love  IKIWA ni siku nyingine mpya kabisa ya Jumatatu baadhi...

error: Content is protected !!