Thursday , 25 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mwandishi wa habari ajitosa ubunge Iringa
Habari za Siasa

Mwandishi wa habari ajitosa ubunge Iringa

Spread the love

MWANDISHI wa habari nchini Tanzania, Tumain Msowoya amechukua fomu ya kuwania ubunge viti maalum kupitia Umoja wa Wanawake Tanzania kupitia Chama Cha Mapinduzi (UWT) Mkoa wa Iringa. Anaripoti Mwandishi Wetu, Iringa…(endelea)

Tumain amekabidhiwa fomu hizo leo Jumanne tarehe 14 Julai 2020 na Katibu wa UWT Mkoa wa Iringa, Angela Milembe katika Ofisi za CCM mkoani humo.

Mwandishi huyo wa habari amewahi kuwa Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa chama hicho (UVCCM) Mkoa wa Iringa.

Baada ya kumkabidhi fomu, MIlembe ametoa wito kwa wanawake kujitokeza kuchukua fomu kwani bado zipo.

Tumain ambaye kwa sasa ni Afisa Habari wa Kampuni ya  kuzalisha nguzo za umeme ya Qwihaya amewahi kutunukiwa tuzo ya heshima ya udaktari kutoka Chuo Kikuu cha The African Graduate cha nchini Sierra Leone

Alitunukiwa kutokana na kazi za uandishi wa habari hasa zilizohusisha masuala ya wanawake, watoto na watu wenye ulemavu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

Mpwa wa Magufuli mbaroni kwa kusambaza picha za utupu

Spread the loveJESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limewakamata...

error: Content is protected !!