Thursday , 28 March 2024
Home Habari Mchanganyiko Mwandishi TBC afariki dunia
Habari Mchanganyiko

Mwandishi TBC afariki dunia

Spread the love

MWANDISHI wa Habari wa Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC), Elisha Elia amefariki dunia katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH). Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea). 

Mkurugenzi Mkuu wa TBC, Dk. Ayub Rioba amesema, Elia amefikwa na mauti leo Jumamosi tarehe 24 Oktoba 2020 alipokuwa amelazwa hospitalini hapo kwa matobabu.

Dk. Rioba amesema,taarifa zaidi zitatolewa.

 

Kwa upande wake, Msemaji Mkuu wa Serikali ya Tanzania, Dk. Hassan Abbas, ametumia ukurasa wa Twitter kuomboleza kifo hicho cha Elia.

“Kwa niaba ya Serikali, tumepokea kwa masikitiko kifo cha Mtangazaji mahiri wa TBC, Elisha Elia, kilichotokea leo Dar es Salaam.”

Dk. Abbas ambaye pia ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo amesema,”Elisha atakumbukwa kwa kipaji chake adhimu katika uandishi wa habari za magazeti na baadaye kuwa mtangazaji galacha.”

1 Comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wafanyabiashara, wawekezaji China waridhia kuwekeza bil. 800 katika sekta 5 nchini

Spread the loveUJUMBE wa wafanyabiashara na wawekezaji wakubwa kutoka Jimbo la Changzhou...

Habari Mchanganyiko

Bil. 4.42 kumaliza uhaba maji kata 2 Musoma Vijijini

Spread the loveWANANCHI wa kata za Busambara na Kiriba, Jimbo la Musoma...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Soko nepi za watoto lashuka, watu wazima lapaa

Spread the loveKiwanda cha kutengeneza nepi cha Japan kimetangaza kuwa kitaacha kutengeneza...

Habari Mchanganyiko

NMB yafuturisha Dar, Majaliwa azitaka Serikali za Mitaa, Taasisi zijifunze kwao

Spread the loveBENKI ya NMB imewafuturisha wateja wake walio kwenye Mfungo wa...

error: Content is protected !!