MWANDISHI wa habari wa AZAM TV, Baruan Muhuza amechukua fomu kuomba ridhaa ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimpitishe kuwania ubunge Kigoma Mjini katika Uchaguzi Mkuu Oktoba 2020. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea)
Barua amechukua fomu leo Jumatano tarehe 15 Julai 2020 Ofisi za CCM Wilaya ya Kigoma.
Jimbo hilo lilikuwa likiongozwa na Zitto Kabwe wa ACT-Wazalendo ambaye mpaka sasa hajaweka wazi kama atagombea tena kwenye uchaguzi mkuu huo.
Mara baada ya kuchukua fomu, Baruani amekishukuru chama hicho kwa kutoa fursa kwa kila mwanachama mwenye sifa kuwania ubunge.
“Nakishukuru chama changu na hii ni ndoto yangu ya kwenda kuwatumikia wananchi wa Kigoma mjini,” amesema Baruan
Leave a comment