Saturday , 20 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Mwanafunzi afariki kwa kujinyonga Mwanza
Habari Mchanganyiko

Mwanafunzi afariki kwa kujinyonga Mwanza

Kitanzi cha kunyonga
Spread the love

ALIYEKUWA Mwanafunzi wa kidato cha tano katika shule ya Sekondari Sengerema mkoani Mwanza, Ayoub Yahya (19) amekutwa amefariki dunia baada ya kujinyonga asubuhi ya leo. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Tukio hilo limethibitishwa leo tarehe 18 Oktoba 2018 na Kaimu Kamanda wa Polisi mkoa wa Mwanza, ACP Advera Bulimba.

ACP Bulimba ameeleza kuwa, mwanafunzi huyo alijinyonga kwa kutumia kamba ya chandarua aliyokuwa ameifunga kwenye mti uliopo pembeni ya uwanja wa mpira wa shule ya Sekondari Sengerema.

Ameeleza kuwa, wanafunzi wenzie ndiyo waliotoa taarifa baada ya kupita uwanjani hapo na kumuona akiwa amefariki kisha wakatoa taarifa kwenye uongozi wa shule ambao ulifikisha taarifa za tukio hilo katika kituo cha polisi.

“Chanzo cha mauaji hayo bado hakijafahamika, Polisi bado tunaendelea na uchunguzi kuhusiana na tukio hilo. Mwili wa marehemu umehifadhiwa hospitali ya DDH Sengerema kwa ajili ya uchunguzi, pindi uchunguzi ukikamilika utakabidhiwa kwa ndugu wa marehemu kwa ajili ya mazishi,” amesema ACP Bulimba.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wauguzi, madaktari 1000 kugawiwa mitungi ya Oryx Gas

Spread the loveKAMPUNI ya Oryx Gas na Taasisi ya Doris Mollel Foundation...

Habari Mchanganyiko

Tanzania yachaguliwa Makamu wa Rais Tume ya Shirika la Hali ya Hewa Duniani

Spread the love  TANZANIA kupitia Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA)...

Habari Mchanganyiko

NEMC yaonya wanaojenga bila tathmini ya mazingira

Spread the loveBARAZA la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC),...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB Pesa Akaunti yawavutia wakaguzi wa ndani Afrika

Spread the loveUbunifu wa bidhaa bora wa Benki ya NMB pamoja na...

error: Content is protected !!