Tuesday , 19 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mwalimu apendekezwa mgombea mwenza urais Chadema
Habari za Siasa

Mwalimu apendekezwa mgombea mwenza urais Chadema

Spread the love

BARAZA Kuu la Chama cha Demokrasia na Maendelea (Chadema) kimependekeza kwa mkutano mkuu wa chama hicho, Salum Mwalimu kuwa mgombea mwenza wa urais wa Tanzania katika Uchaguzi Mkuu utakaofanyika Jumatano tarehe 28 Oktoba 2020. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam…(endelea)

Mwalimu ambaye ni Naibu Katibu Mkuu wa Chadema-Zanzibar amependekezwa leo Jumatatu tarehe 3 Agosti 2020 na kesho Jumanne atathibitishwa na mkutano mkuu.

Akizungumza mbele ya wajumbe wa mkutano huo, Mwaimu ambaye kitaaluma ni mwandishi wa habari amesema, amejiandaa vyema kwenda kuhakikisha anapambana ili mgombea urais atangazwe baada ya uchaguzi kufanyika.

Mwalimu amesema yeye ni “mtoto wa Chadema ambaye sijawahi kuwa mwanachama wa chama chochote. Nimelelewa na chama hiki. Niko tayari kutumwa.”

Mwaimu amesema, jukumu hilo ni zito na matumaini yake, familia na watoto “wangu wananielewa kwani mgombea wetu kushinda atashinda ila kutangazwa tutahakikisha ametangazwa.”

Kura za wazi na wajumbe 456 zilipopigwa, watano walisema hapana na wengine ndio.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari za Siasa

Zanzibar mbioni kuanza uchimbaji mafuta na gesi baharini

Spread the loveSERIKALI ya Zanzibar, imekamilisha mchakato wa uchimbaji wa mafuta na...

Habari za Siasa

Wizara ya afya yataja mafanikio 10 miaka mitatu Samia madarakani

Spread the loveWIZARA ya Afya imetaja mafanikio 10 iliyoyapata ndani ya miaka...

Habari za Siasa

Mbozi walilia kuwa manispaa, majimbo 3

Spread the loveHALMASHAURI ya wilaya ya Mbozi mkoani Songwe imeeleza dhamira yake...

Habari za Siasa

Wabunge waitaka TPDC kuongeza kasi ya kuunganisha wateja gesi asilia

Spread the love  KAMATI ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini...

error: Content is protected !!