MJENGI Samson, Mwalimu wa Shule ya Msingi Isomya, Manispaa ya Singida, amehukumiwa kifungo cha miaka 30 jela kwa kumbaka na kumjaza mimba mwanafunzi wa darasa la sita katika shule hiyo. Anaripoti Mwandishi Wetu, Singida … (endelea).
Hukumu hiyo imetolewa na Aristida Tarimo, Hakimu Mfawidhi wa Wilaya baada ya mwalimu huyo kutiwa hatiani pasipo na shaka.
Samson amehukumiwa kwa makosa mawili ambapo, kosa la kwanza, ni la kumbaka mtoto huyo hivyo ametupwa jela kwa miaka 30, kosa la pili ni kumjaza mimba ambapo amefungwa miaka miwili, adhabu hizo zitaenda sambamba.
Patricia Mkina ambaye ni mwendesha mashtaka wa mahakama hiyo ameeleza, katika shauri hilo la jinai, tukio la kwanza lilifanyika kati ya tarehe 4 Aprili 2019 na Julai 2019.
Mkina ameleza, Samason alimfanyia unyama mwanafunzi huyo mwenye umri wa miaka 16 katika Kijiji cha Isonya, Kata ya Mwankoko.
Awali, mshtakiwa alikana kutenda kosa hilo, lakini baada ya kupelekwa ushahidi ikiwa ni pamoja na mwanafunzi mwenyewe kuieleza mahakama, mtuhumiwa huyo alikuwa akimpeleka vichakani kutenda tendo hilo.
Na hata baada ya kupimwa na madaktari kama alikuwa na ujauzito, mtoto huyo alipoulizwa muhusika, alimtaja mwalimu huyo.
“Baadaya kumtaja mwalimu Samson kwamba ndiye aliyehusika, wazazi wake walikwenda kutoa taarifa kwa mtendaji kata, mkuu wa shule na kituo cha polisi,” ameeleza Mkina.
Leave a comment