Friday , 29 March 2024
Home Habari Mchanganyiko Mwalimu amjaza mimba ‘denti’ afungwa miaka 30
Habari Mchanganyiko

Mwalimu amjaza mimba ‘denti’ afungwa miaka 30

Spread the love

MJENGI Samson, Mwalimu wa Shule ya Msingi Isomya, Manispaa ya Singida, amehukumiwa kifungo cha miaka 30 jela kwa kumbaka na kumjaza mimba mwanafunzi wa darasa la sita katika shule hiyo. Anaripoti Mwandishi Wetu, Singida … (endelea).

Hukumu hiyo imetolewa na Aristida Tarimo, Hakimu Mfawidhi wa Wilaya baada ya mwalimu huyo kutiwa hatiani pasipo na shaka.

Samson amehukumiwa kwa makosa mawili ambapo, kosa la kwanza, ni la kumbaka mtoto huyo hivyo ametupwa jela kwa miaka 30, kosa la pili ni kumjaza mimba ambapo amefungwa miaka miwili, adhabu hizo zitaenda sambamba.

Patricia Mkina ambaye ni mwendesha mashtaka wa mahakama hiyo ameeleza, katika shauri hilo la jinai, tukio la kwanza lilifanyika kati ya tarehe 4 Aprili 2019 na Julai 2019.

Mkina ameleza, Samason alimfanyia unyama mwanafunzi huyo mwenye umri wa miaka 16 katika Kijiji cha Isonya, Kata ya Mwankoko.

Awali, mshtakiwa alikana kutenda kosa hilo, lakini baada ya kupelekwa ushahidi ikiwa ni pamoja na mwanafunzi mwenyewe kuieleza mahakama, mtuhumiwa huyo alikuwa akimpeleka vichakani kutenda tendo hilo.

Na hata baada ya kupimwa na madaktari kama alikuwa na ujauzito, mtoto huyo alipoulizwa muhusika, alimtaja mwalimu huyo.

“Baadaya kumtaja mwalimu Samson kwamba ndiye aliyehusika, wazazi wake walikwenda kutoa taarifa kwa mtendaji kata, mkuu wa shule na kituo cha polisi,” ameeleza Mkina.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Puma Energy Tz: Watanzania tudumishe amani kuvutia uwekezaji

Spread the loveKAMPUNI ya Mafuta ya Puma Tanzania imewakutanisha wadau mbalimbali katika...

Habari Mchanganyiko

DAWASA waanza utekelezaji agizo la Samia

Spread the loveMamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam...

Habari MchanganyikoKimataifa

Zuma akataliwa kugombea urais

Spread the loveTUME Huru ya Uchaguzi Afrika Kusini (IEC) imemwondoa rais wa...

Habari Mchanganyiko

Mtandao watetezi wa haki za mazingira Tanzania waundwa

Spread the loveMTANDAO wa watetezi wa haki za mazingira nchini Tanzania, umeundwa...

error: Content is protected !!