Friday , 29 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mwakyembe atoa sababu 10 za kuhamia CCM
Habari za Siasa

Mwakyembe atoa sababu 10 za kuhamia CCM

Spread the love

ALIYEKUWA Diwani wa Mtoni kwa tiketi ya CHADEMA, Bernard Mwakyembe, ametoa sababu 10 zilizomfanya aondoke Chadema na kuhamia CCM. Anaripoti Gerva Lyenda … (endelea).

Mwakyembe alizitaja sababu hizo mbele ya Waandishi wa habari leo Jumamosi tarehe 29 Septemba kwenye mkutano na vyombo vya habari alioufanya jijini Dar es Salaam.

Mwakyembe alizitaja sababu hizo kuwa ni kasi ya kufanya maendeleo inayofanywa na Serikali, agenda za Chadema kutekelezwa na Serikali, kujengwa miundombinu, ujenzi wa mradi wa Stigler’s Gorge, reli ya standard gauge na kushughulika na mafisadi kunakofanywa na Serikali.

Alizitaja sababu nyingine kuwa ni kuondolewa watumishi hewa makazini, ununuzi wa ndege, kupunguza matumizi ya Serikali na kuboresha huduma za hospitali ya Muhimbili ambapo sasa watu hawaendi nje ya nchi kutafuta matibabu bora.

Mwanasiasa huyo anayedai kuwa alikuwa msaidizi wa Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe, alijiunga na CCM Septemba 15 mwaka huu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

error: Content is protected !!