MZEE Jumanne Ngoma, mvumbuzi wa Tanzanite amefariki dunia. Anaripoti Bupe Mwakiteleko … (endelea).
Taarifa ya familia yake inaeleza kuwa Mzee Ngoma alifariki dunia wakati akipatiwa matibabu katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili jana jioni tarehe 31 Januari 2019.
Utaratibu wa mazishi ya mvumbuzi huo mwenye umri wa miaka 80 bado hayajapangwa.
Mwanaye Hassan Ngoma ameeleza kuwa, taratibu zaidi zitajulikana hapo baadaye.
Mwaka jana tarehe 6 Aprili Rais John Magufuli wakati wa uzinduzi wa ujenzi wa ukuta unaozunguka mgodi wa Tanzanite, alimzawadia Sh. 100 mil kutokana na mchango wake kwenye madini hayo.
Leave a comment