WAZIRI wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu amemsimamisha kazi Abednego Alfred, Muuguzi katika Kituo cha Afya cha Mamba, anayetuhumiwa kumbaka mama mjazito. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).
Waziri Ummy amechukua hatua hiyo leo tarehe 20 Desemba 2019, akiwa wilayani Mpanda, Mkoa wa Rukwa.
Aidha, Waziri Ummy ameliagiza Baraza la Wauguzi na Ukunga nchini, kusimamisha leseni ya Alfred, wakati uchunguzi wa tuhuma dhidi yake, ukiendelea kufanyika.
“Naliagiza baraza la wauguzi na ukunga kusimamisha leseni ya muuguzi huyu, wakati uchunguzi unafanyika,” ameagiza Waziri Ummy.
Wakati huo huo, Waziri Ummy amewaonya watumishi wa afya kutokiuka viapo vya maadili yao ya kazi na sheria.
“Na yeyote atakayefanya kazi kinyume na maadili, weledi na kiapo chake tutamchukulia hatua za kinidhamu. Ikewemo kuwafutia leseni zao na kuwapeleka katika vyombo vya dola”Amesisitiza Waziri Ummy.
Tukio linadaiwa kutokea tarehe 18 Desemba 2019, ambapo mAlfred anadaiwa kumbaka mama mjazito aliyekwenda katika Kituo cha Afya cha Mamba, kwa ajili ya kupata huduma ya kujifungua.
Inadaiwa kuwa, wakati mama mjazito huyo akiugulia maumivu ya uchungu, ndipo mtuhumiwa alipoitumia nafasi hiyo kumuingilia, hali iliyomfanya mama huyo kushtuka, ndipo alipomuona Alfred anamfanyia kitendo hicho cha ukatili.
Leave a comment