Saturday , 20 April 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa ‘Muuaji msikitini New Zealand alijaza silaha kwenye gari lake’
Kimataifa

‘Muuaji msikitini New Zealand alijaza silaha kwenye gari lake’

Spread the love

BRENTON Tarrant (28) aliyeshiriki kufanya mauaji msikitini nchini New Zealand jana tarehe 15 Machi 2019 na kusababisha vifo vya waumini wa dini ya kiislam 49, amekutwa na silaha nyingi kwenye gari alilotumia. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa … (endelea).

Uchunguzi wa awali uliofanywa na Jeshi la Polisi nchini humo umeeleza kuwa, Tarrant ambaye ni raia wa Australia ameshiriki kwenye mauaji hayo ya kikatili katika Mji wa Christchurch tayari amefikishwa mahakamani.

Jacinda Arden, Waziri Mkuu wa New Zealand akizungumza na vyombo vya habari leo tarehe 16 Machi 2019 amesema, uchunguzi wa awali unaonesha kwamba, Tarrant alitoka na bunduki tano kwenye gari hilo.

Amesema, bunduki zilizotumiwa na mtuhumiwa katika kutekeleza shambulio hilo zilikuwa zimebadilishwa ambapo gari lake alikuwa amelijaza silaha pamoja na leseni za silaha.

Tarrant ameendelea kuwekwa kizuizini baada ya kunyimwa dhamana na kwa mara nyingine anatarajiwa kupandishwa kizimbani tarehe 5 Aprili mwaka huu.

Wakati Tarrant akifunguliwa shitaka la peke yake la mauaji, watuhumiwa wengine watatu akiwemo mwanamke mmoja na wanaume wawili wanaendelea kuwekwa kizuini na Jeshi la Polisi nchini humo.

Waziri Arden amesema, serikali ya New Zealand itatoa msaada wa kifedha kwa familia zilizopoteza ndugu zao katika tukio hilo.

Meya wa Mji wa Christchurch ambako kulitokea tukio hilo jana alfajiri, Lianne Dalziel amesema bendera zilizoko katika majengo ya serikali zitasimamishwa nusu mlingoti hadi pale taarifa zaidi zitakapotolewa.

Tukio hilo la kusikitishalililopoteza maisha ya watu 49 na kuacha majeruhi 48, lilitokea katika misikiti miwili- Lin Wood na Al Noor.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the loveMajaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa...

Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the loveSpika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu...

Habari MchanganyikoKimataifa

Tetemeko la ardhi laua 7, lajeruhi 800 Taiwan

Spread the loveWatu wapatao saba wamefariki dunia na wengine zaidi ya 800...

error: Content is protected !!