MUFTI wa Tanzania, Aboubakar Zubeir amefiwa na mke wake mkubwa anayefahamika kwa jina la Mama Shafi. Anaripoti Regina Mkonde … (endelea).
Taarifa ya kifo hicho imetolewa leo tarehe 30 Jnauari 2019 na Mwenyekiti wa Halmashauri Kuu Baraza Kuu la Waislamu Tanzania (BAKWATA), Sheikh Hamis Mataka.
Taarifa ya Sheikh Mataka inaeleza kuwa, Mama Shafi amefariki dunia akiwa wilaya ya Korogwe mkoani Tanga.
Mazishi ya Mama Shafi yatafanyika kesho tarehe 31 Januari 2019 baada ya swala ya adhuhuri mkoani Tanga.
Leave a comment