Friday , 29 March 2024
Home Habari Mchanganyiko Mtuhumiwa azidunda kortini kupinga masharti ya dhamana
Habari Mchanganyiko

Mtuhumiwa azidunda kortini kupinga masharti ya dhamana

Daniel Njonjo, Mtuhumiwa wa shtaka la kufanya vurugu Kenya
Spread the love

DANIEL Njonjo, anayetuhumiwa kwa shtaka la kufanya vurugu, amepigana na polisi katika korti ya Mahakama ya Milimani jijini Nairobi, Kenya, akipinga sharti la dhamana. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa…(endelea).

Kisa hicho kimetokea jana tarehe 8 Januari 2020, baada ya Hakimu Mkazi Mkuu wa mahakama hiyo, Muthoni Nzibe, kumuamuru mtuhumiwa huyo kutoa Shilingi ya Kenya 30,000, kama sharti la dhamana.

Baada ya mahakama kutoa sharti hilo, Njonjo alianza vurugu na kupelekea kupigana na maafisa polisi wa mahakama hiyo, waliojaribu kumkamata kwa ajili ya kumpeleka rumande.

Katika utetezi wake, Njonjo alisema ni bora afe kuliko kutekeleza sharti hilo, kwa kuwa hana uwezo wa kutoa kiasi hicho cha fedha.

Na kuiomba mahakama hiyo kumuacha kwa dhamana, kwa kuwa hakumuuwa mtu.

Njonjo anatuhumiwa kukutwa na kisu katika Mtaa wa Kimathi jijini Nairobi, Kenya. Na anatarajiwa kurudi tena mahakamani hapo tarehe 22 Januari mwaka huu, siku ambayo kesi yake itakwenda kutajwa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Puma Energy Tz: Watanzania tudumishe amani kuvutia uwekezaji

Spread the loveKAMPUNI ya Mafuta ya Puma Tanzania imewakutanisha wadau mbalimbali katika...

Habari Mchanganyiko

DAWASA waanza utekelezaji agizo la Samia

Spread the loveMamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam...

Habari MchanganyikoKimataifa

Zuma akataliwa kugombea urais

Spread the loveTUME Huru ya Uchaguzi Afrika Kusini (IEC) imemwondoa rais wa...

Habari Mchanganyiko

Mtandao watetezi wa haki za mazingira Tanzania waundwa

Spread the loveMTANDAO wa watetezi wa haki za mazingira nchini Tanzania, umeundwa...

error: Content is protected !!