MAANDAMANO yameibuka jimbo la Wisconsin nchini Marekani baada ya polisi kutuhumiwa kumpiga risasi mtu mweusi nchini humo, Jacob Blake. Inaripoti BBC…(endelea)
Video zilizosambaa kwenye mitandao ya kijamii zimeonesha Blake akipigwa risasi kwa nyuma wakati anajaribu kuingia kwenye gari katika mji wa Kenosha.
Blake yupo hospitali akiendelea na matibabu huku mamlaka za Kenosha imetangaza hali ya dharura ya watu kutotoka nje baada ya kuzuka kwa maandamano.
Soma zaidi hapa
Mtu mweusi afanyiwa unyama Marekani
Mamia ya watu wameandamana hadi makao makuu ya polisi jana jumapili usiku na kuchoma moto magari huku waandamanaji wakipiga kelele wakisema hawawezi kurudi nyuma.
Tahadhari iliyotolewa kwa umma, polisi wamesema wanaofanya biashara saa 24 wafikirie kuzifunga kwasababu ya wizi na uvunjifu wa amani unaoweza kujitokeza.
Polisi wametumia mabomu ya machozi kutawanya mamia ya waandamanaji waliokiuka kauli ya kutotoka nje.
Gavana wa jimbo la Wisconsin, Tony Evers ameshutumu tukio hilo la kupigwa risasi Blake ambaye inasemekana hakuwa na silaha.
Evers amesema, wakati hana taarifa zote kwa sasa, anachojua ni kwamba huyo sio mtu wa kwanza kupigwa risasi au kujeruhiwa au kuuawa kiholela mikononi mwa polisi katika jimbo lao au nchi yao.
Idara ya haki ya Wisconsin inayochunguza tukio hilo, Imesema maafisa waliohusika wameagizwa kwenda likizo kwa uchunguzi zaidi.
Tukio hilo limetokea ikiwa imepitwa miezi michache tangu Afisa wa polisi mzungu kutuhumiwa kumuua raia wa Marekani, George Floyd.
Afisa huyo, Derek Chauvin aliyemkandamiza kwa mguu wake Floyd kisha kumfanya ashindwe kupumua na kupoteza maisha ameshtakiwa kwa mauaji.
Leave a comment