MWILI wa Rosemary, mtoto wa Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere utazikwa Jumatano hii ya tarehe 6 Januari 2021, makaburi ya Kituo cha Hija, Pungu jijini Dar es Salaam. Anaripoti Brightness Boaz, Dar es Salam … (endelea) .
Rosemary alifikwa na mauti Jumamosi tarehe 01 Januari 2021 katika hospitali ya Mzena, jijini Dar es Salaam alipokuwa amelazwa akipatiwa matibabu kwa muda mrefu.
Mtoto huyo wa mwasisi wa taifa la Tanzania na ambaye aliwahi kuwa mbunge wa Bunge la Muungano, katika Bunge la tisa, aliyezaliwa mwaka 1961, enzi za uhai wake, alisema akifariki azikwe makaburi hayo ya Pugu.
Msemaji wa familia, Bkobe Nyerere alisema, Rosemary enzi za uhai wake aliomba akifariki dunia akazikwe kwenye eneo ambalo wanazikwa wafia dini ambayo hutumika kama sehemu ya hija kwa waumini wa Kikristu hususan wakatoliki.
Kwa sasa msiba uko Msasani jijini Dar es Salaam, nyumbani kwa Mwalimu Nyerere ambako watu mbalimbali wakiwemo viongozi wanakwenda kutoa salamu za pole kwa wafiwa.
Bkoke alisema, mwili wa Rosemary utawasili nyumbani hapo kesho ambapo utalala hapo na Jumatano (keshokutwa) kutakuwa na ibada ya kuaga mwili katika Kanisa la Mtakatifu Imakulata-Upanga na baada ya kumalizika, safari ya kwenda makaburini Pugu itaanza.
Miongoni ni Makamu wa Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan aliyekwenda jana Jumapili.
Leave a comment