Thursday , 25 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Mtoto afariki kwenye ajali ya moto
Habari Mchanganyiko

Mtoto afariki kwenye ajali ya moto

Ulrich Matei Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya
Spread the love

MTOTO mmoja aliyefahamika kwa jina la Chriss Shida (2) amefariki dunia baada ya kuungua na moto akiwa nyumbani kwao katika kijiji cha Kimondo Wilayani Mbeya mjini. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Akizungumza na wanahabari leo tarehe 28 Agosti, 2018 SACP Ulrich Matei, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya amesema tukio hilo lilitokea jana majira ya saa mbili usiku.

Akielezea kuhusu tukio hilo, amesema chanzo cha moto huo ni mabanzi na majani ya jiko kuanguka wakati wahanga wako jikoni wanakula na kusababisha kushika moto na kuwaunguza.

Aidha, Kamanda Matei amesema mama mzazi wa marehemu aitwaye Maria Lucas alijeruhiwa na moto huo sehemu za mikononi na kifuani.

Kamanda Matei amesema mwili wa marehemu umehifadhiwa katika hospitali teule ya Ifisi Mbalizi na mama wa marehemu anapatiwa matibabu hospitalini hapo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

error: Content is protected !!