Friday , 19 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Mtoto (3) afikishwa kortin Jerusalem
Habari Mchanganyiko

Mtoto (3) afikishwa kortin Jerusalem

Spread the love

MOHAMMED Rabi ‘Aliani (3), amefikishwa katika Kituo cha Polisi cha Yerusalem kuhojiwa akituhumiwa kuwapiga mawe wanajeshi wa Israel. Inaripoti mitandao ya kimataifa…(endelea).

Ni baada ya kikosi cha Jeshi la Israel kuvamia makazi yao yaliyopo katika Mji wa Al-Sawiya, Jerusalem ya Mashariki.

Uongozi wa Israeli Jumatatu ya tarehe 29 Julai 2019, ulitoa agizo la kumtaka Rabi afikishwe katika kituo cha polisi cha Yerusalemu ili kuhojiwa na polisi.

Wapalestina wakazi wa Mji wa al-‘Isawiya, walifuatana na mtoto Rabi kwenda kwenye kituo hicho cha polisi huku wakifanya maandamano.

Jumuiya ya Palestina ya kutetea haki za wafungwa, imeomba uchunguzi ufanyike juu ya tukio hilo.

Mkuu wa jumuiya hiyo, Meja Jenerali Kadri Abu Bakr amelaani uongozi wa Israeli kwa kumtaka mtoto huyo wa miaka 3 kuhojiwa kwenye kituo cha polisi, akisisitiza kwamba kitendo hicho ni uhalifu dhidi ya watoto wa Palestina.

Abu Bakr amehoji ukimya wa jumuiya ya kimataifa juu ya ukiukaji wa sheria za kimataifa juu ya Haki za Watoto unaofanywa na Israel. Na kwamba, umesababisha muendelezo wa unyanyasaji na uonevu wa watoto hao.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB Pesa Akaunti yawavutia wakaguzi wa ndani Afrika

Spread the loveUbunifu wa bidhaa bora wa Benki ya NMB pamoja na...

Habari Mchanganyiko

Carbon First, Ruangwa wasaini makubaliano ya biashara ya hewa ukaa

Spread the love  KAMPUNI ya Carbon First Tanzania Limited na Halmashauri ya...

Habari Mchanganyiko

CBE yawakumbuka wenye mahitaji maalum Jangwani

Spread the loveCHUO cha Elimu ya Biashara (CBE), kimetoa msaada mbalimbali na...

Habari Mchanganyiko

Mume auwa mke kwa kumchoma visu, ajisalimisha Polisi

Spread the loveJACKSON Kalamji (49), anashikiliwa na Jeshi la Polisi jijini Mwanza,...

error: Content is protected !!