Saturday , 20 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mtolea aonja jeuri ya upinzani bungeni
Habari za SiasaTangulizi

Mtolea aonja jeuri ya upinzani bungeni

Abdallah Mtolea, aliyekuwa Mbunge wa Temeke
Spread the love

ABDALLAH Mtolea, Mbunge wa Temeke ameapishwa leo tarehe 29 Januari 2019 bungeni mbele ya wabunge wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) na wa CUF Kambi ya Prof. Ibrahim Lipumba pekee. Anaripoti Danson Kaijage, Dodoma … (endelea).

Mtolea ameapishwa leo baada ya kupita bila kupingwa kwenye uchaguzi wa marudio uliofanyika mwishoni mwa Disemba mwaka jana kwenye jimbo hilo. Mbunge huyo awali aliiwakilisha CUF kwenye lakini tarehe 15 Novemba mwaka jana alijiuzulu.

Wakati akiingia bungeni kuapishwa, wapinzani hawakuwemo, walisubiri baada ya kuapishwa kwake ndio wakaingia bungeni wakionesha kutomuunga mkono kwa hatua yake ya kujiunga na ‘mpinzani’ wao.

Tofauti na ilivyo kawaida ya wabunge waliojiunga na CCM wakitokea upinzani, mbwembwe zilizozoeleka za kuwasindikiza waliojunga nao zilikuwa hafifu. Mtolea aliyevalia suti ya bluu alisindikizwa na chereko chache na kisha kuapishwa na Job Ndugai, Spika wa Bunge la Jamhuri.

Baada ya kuapishwa Mtolea alikwenda kumsalimia Waziri Mkuu, Kasim Majaliwa; Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Prof. Adelardus Kilangi na Waziri wa Ofisi ya Waziri Mkuu, Jenister Mhagama.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Dk. Mwakyembe : Zanzibar waliongoza kutaka Serikali 2 za muungano

Spread the love  MWANASIASA mkongwe nchini, Dk. Harrison Mwakyembe, amesema mjadala wa...

Habari za SiasaTangulizi

Rais Samia ataja mikakati ya kufikia trilioni 2 biashara Uturuki, Tz

Spread the loveWakati Tanzania na Uturuki zikidhamiria kuongeza kiwango cha biashara hadi...

BiasharaHabari za Siasa

Mavunde aagiza Perseus kuharakisha fidia Sengerema

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameipongeza Kampuni ya Perseus kwa...

Habari za Siasa

Kigogo Chadema awanyooshea vidole vigogo serikalini kuhusu ripoti ya CAG

Spread the love  MWANACHAMA wa Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Boniface Jacob, amedai...

error: Content is protected !!