ABDALLAH Mtolea, Mbunge wa Temeke ameapishwa leo tarehe 29 Januari 2019 bungeni mbele ya wabunge wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) na wa CUF Kambi ya Prof. Ibrahim Lipumba pekee. Anaripoti Danson Kaijage, Dodoma … (endelea).
Mtolea ameapishwa leo baada ya kupita bila kupingwa kwenye uchaguzi wa marudio uliofanyika mwishoni mwa Disemba mwaka jana kwenye jimbo hilo. Mbunge huyo awali aliiwakilisha CUF kwenye lakini tarehe 15 Novemba mwaka jana alijiuzulu.
Wakati akiingia bungeni kuapishwa, wapinzani hawakuwemo, walisubiri baada ya kuapishwa kwake ndio wakaingia bungeni wakionesha kutomuunga mkono kwa hatua yake ya kujiunga na ‘mpinzani’ wao.
Tofauti na ilivyo kawaida ya wabunge waliojiunga na CCM wakitokea upinzani, mbwembwe zilizozoeleka za kuwasindikiza waliojunga nao zilikuwa hafifu. Mtolea aliyevalia suti ya bluu alisindikizwa na chereko chache na kisha kuapishwa na Job Ndugai, Spika wa Bunge la Jamhuri.
Baada ya kuapishwa Mtolea alikwenda kumsalimia Waziri Mkuu, Kasim Majaliwa; Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Prof. Adelardus Kilangi na Waziri wa Ofisi ya Waziri Mkuu, Jenister Mhagama.
Leave a comment