Saturday , 20 April 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Mtindo mpya wa maisha New York
Kimataifa

Mtindo mpya wa maisha New York

Spread the love

TISHO la virusi vya corona limebadili utaratibu wa maisha duniani. Mfano ulio wazi ni Jiji la New York, Marekani wikiendi iliyopita. Inaripoti mitandao ya kinataifa … (endelea).

Eneo ambalo watu walikuwa wakienda kustarehe kwa michezo mbalimbali, sasa limezungushiwa viduara na kwa anayetaka kuwepo eneo hilo, anapaswa kukaa ndani ya duara lake.

Hakuna uhuru wa kutembeatembea, kula wala kunywa eneo hilo, wanaofika pale kwa sasa wanaruhusiwa ‘kupiga stori’ tu ndani ya kiduara chao walichokikuta na kisha kuondoka.

Maisha katika viwanja vya ‘Domino Park’, yamebadilika, sasa hakuna kurukaruka na michezo ya hapa na pale, hakuna kupigana vikumbo, utii wa umbali wa mita sita umezingatiwa.

Viwanja vya Domino Park ni maarufu sana jijini humo kwa watu kukutana na kupumzika, majani yaliyopandwa na kutunzwa vizuri, mwanga wa kutosha na utulivu wake uliwafanya wakazi wa jiji hilo kuzuru mara kwa mara.

Kila wikiendi, eneo hilo lilikuwa limejaa watu wa aina mbalimbali, ni eneo linalovutia wapenzi kwenda kupumzika na hata ahadi ya makutano kutokana na umaarufu wake.

Viduara vilivyozungushwa kwenye viwanja hivyo, vina futi sita vikitosha watu wawili mpaka wanne. Lengo ni kuendelea na kupambana na maambukizi mapya ya virusi vya corona kwakuwa umbali unaokubalika.

Jiji hilo ambalo limeripoti zaidi ya visa 200,000, licha ya masharti ya kukaa ndani kulegezwa, wakazi wa New York wameshauriwa kuendelea kukaa ndani iwapo hawana ulazima wa kutoka.

Mtindo wa kuweka alama kutoka mtu na mtu umeimarishwa maeneo malimbali ikiwa ni pamoja na madukani, ofisini, hotelini, migahawani na sehemu za biashara.

Mpaka sasa, Marekani ndio taifa la kwanza linaloogoza kwa  wagonjwa zaidi ya 1.4 milioni wa corona na vifo vilivyotokana na ugonjwa huo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the loveMajaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa...

Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the loveSpika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu...

Habari MchanganyikoKimataifa

Tetemeko la ardhi laua 7, lajeruhi 800 Taiwan

Spread the loveWatu wapatao saba wamefariki dunia na wengine zaidi ya 800...

error: Content is protected !!