Wednesday , 24 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Mtanzania awa Mwafrika wa kwanza kutwaa tuzo ya Brady
Habari MchanganyikoKimataifa

Mtanzania awa Mwafrika wa kwanza kutwaa tuzo ya Brady

Joyce Singano
Spread the love

 

JOYCE Singano, mwanasayansi na mtafiti, amekuwa Mwafrika wa kwanza kutwaa tuzo maarufu inayotolewa kwa wataalamu wa maiamba duniani ‘Brady Meda.’ Inaripoti mitandao ya kimataifa … (endelea).

Brady Medal ndio tuzo kubwa zaidi duniani inayotolewa kwa watafiti waliofanya vizuri kwa mwaka husika. Singano ameibuka kinara wa utafiti kwa mwaka 2020.

Singano mwenye mchango mkubwa katika Shirika la Maenedeleo la Petroli Tanzania (TPDC),ametwaa tuzo hiyo kubwa zaidi miongoni mwa tuzo zinazotolewa kwa watafiti wa ukadiriaji wa miamba wanaotumia visukuku viumbe ambao wanapatikana ardhini.

“…ni kwamba kwa mwaka ule wa 2020, walikuja na wenzako wote wakatathminiwa, wewe ukaonekana unastahili kupata tuzo hiyo.

“Kwangu mimi ni heshima kubwa mno ambayo sikuitegemea kabisa, na hasa ukitazama research (tafiti) wanazotazama hivi karibuni, hawatazami research ya mwaka mmoja na hawatazami faida ya mtu mmoja mmoja, wanatanzama je umesaidia watu wangapi katika hiyo research yako na dunia imefaidikaje?” ameeleza Singano ambaye ni mstaafu kwa miaka 10 sasa.

Amesema, alidokezwa kwamba ushindi wake unatokana na kazi alizowahi kufnya tangu mwaka 1999 mpaka 2009, na kwamba zimeonekana kuwa na mchango mkubwa kwa watu wengi walipitia kwake.

‘Brady Medal’ ni nini?

Hii ndio tuzo ya juu zaidi ya Jumuiya ya Wanasaansi watafiti (Micropalaeontological). Imeanzishwa kwa heshima ya wanasayansi watafiti George Stewardson Brady (1832-1921) na Henry Bowman Brady (1835-1891) kwa kutambua mchango wao kwenye utafiti kupitia viumbe asili.

Medali hiyo hutoleewa kwa wanasayansi ambao wamekuwa na ushawishi mkubwa kupitia tafiti zao. Huduma kwa jamii ya kisayansi pia huwa sehemu ya sababu ya kuzingatiwa na kamati ya tuzo hiyo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

THRDC yaongeza mkataba wa ushirikiano na ABA

Spread the love  MTANDAO wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC),...

Habari Mchanganyiko

Rufaa ya Equity Benki, State Oil yakwama

Spread the loveMAHAKAMA ya Rufani, jijini Dar es Salaam, imeshindwa kuendelea na...

Habari Mchanganyiko

Bodaboda waeleza mafanikio mafunzo usalama barabarani

Spread the loveMADEREVA bodaboda katika Jiji la Dodoma wameeleza jinsi mafunzo ya...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NBC yaahidi kuendelea kuunga mkono Serikali za Mitaa

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) imesisitiza dhamira yake ya...

error: Content is protected !!