Tuesday , 19 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Msajili avitaka vyama vya siasa kuzingatia sheria
Habari za Siasa

Msajili avitaka vyama vya siasa kuzingatia sheria

Msajili msaidizi wa vyama vya siasa, Sisty Nyahonza
Spread the love

OFISI ya Msajili wa Vyama vya Siasa nchini Tazania, umetoa wito kwa vyama vya siasa nchini humo kuhakikisha wanazingatia sheria na taratibu. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam…(endelea).

Kauli hiyo imetolewa na Msajili msaidizi wa vyama vya siasa, Sisty Nyahonza mbele ya wajumbe wa mkutano mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) unaofanyika ukumbi wa Mlimani City, Dar es Salaam.

Hata hivyo, Nyahoza amekutana na kauli za wajumbe zilizokuwa zikikatisha hotuba yake.

“Nimehudhuria mkutano huu mara kadhaa na nipo hapa kumwakilisha msajili wa vyama na sisi tunakuja hapa kutekeleza wajibu wetu wa kisheria wa vyama vyote,” amesema Nyahoza huku sauti zikisikika zikisema ‘mbona msajili mwenyewe hatumwoni’

Akiendelea, Nyahoza amesema “ili kuhakikisha mikutano yenu inafanyika kwa kuzingatia sheria na kanuni. Kwenye haki kuna wajibu ikiwemo kusimamia sheria za nchi.”

Kisha sauti zikasikika zikisema ‘mbona kuna sheria mbovu.’

“Mwenyekiti (Freeman Mbowe), moja wapo ya misingi muhimu ya chama cha siasa, kama mnavyosema mnatetea demokrasia, msingi muhimu ni demokrasia ndani ya chama na demokrasia ni sehemu ya watu kuheshimu sheria.”

Akihitimisha hotuba yake, Nyahoza amesema “wito wetu kama ofisi ya msajili na mlezi, ninyi na vyama vyote mheshimu sheria na tunashauri tuheshimu sheria, tufanye uchaguzi kwa uhuru, haki na amani.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari za Siasa

Zanzibar mbioni kuanza uchimbaji mafuta na gesi baharini

Spread the loveSERIKALI ya Zanzibar, imekamilisha mchakato wa uchimbaji wa mafuta na...

Habari za Siasa

Wizara ya afya yataja mafanikio 10 miaka mitatu Samia madarakani

Spread the loveWIZARA ya Afya imetaja mafanikio 10 iliyoyapata ndani ya miaka...

Habari za Siasa

Mbozi walilia kuwa manispaa, majimbo 3

Spread the loveHALMASHAURI ya wilaya ya Mbozi mkoani Songwe imeeleza dhamira yake...

Habari za Siasa

Wabunge waitaka TPDC kuongeza kasi ya kuunganisha wateja gesi asilia

Spread the love  KAMATI ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini...

error: Content is protected !!