WAZIRI wa Maliasili na Utalii, Dkt. Hamisi Kigwangalla amepata ajali alfajiri ya leo tarehe 4 Agosti, 2018 kwenye eneo la Magugu mkoani Manyara akiwa safarini akitokeaArusha kuelekea Dodoma. Anaripoti Regina Kelvin…(endelea).
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Manyara, Augustino Senga amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo ambapo amesema Afisa wa Habari wa Wizara hiyo, Hamza Temba aliyekuwa kwenye msafara wa waziri amefariki dunia.
Naye Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha, RPC Ramadhan Ng’azi Rpc amethibitisha taarifa za ajali hiyo ambapo amesema Waziri Kigwangalla amepata ajali hiyo Mkoani Manyara alipokuwa njiani akitokea Arusha kuelekea Dodoma.
“Ajali alipata mkoani Manyara, alikuwa Arusha kikazi akaondoka alfajiri kuelekea safari yake nafikiri Dodoma alipofika Manyara tukapewa taarifa kwamba amepata ajali,” amesema RPC Ng’azi.
Nilikuwa njiani nakwenda Babati nimefanikiwa kumsalimia Mh Waziri Kigwangala kituo cha afya Magugu ,anaweza kuongea ni uhakika kuwa Mungu atamponya haraka ,sala dua na maombi ni muhimu kwa wote waliokutwa na ajali hii mbaya.
— Godbless E.J. Lema (@godbless_lema) August 4, 2018
Taarifa zinasema Dk. Kigangwalla anaendelea vizuri na anapelekwa hospitali ya Mount meru Arusha pamoja na msaidizi wake ambaye ameumia sana kwa kutumia helkopta kutoka Magugu.
Leave a comment