Thursday , 28 March 2024
Home Habari Mchanganyiko MPFCR: Vijana jiepusheni na mihadarati
Habari Mchanganyiko

MPFCR: Vijana jiepusheni na mihadarati

Waathirika wa dawa za kulevya wakishiriki uandaji wa miti Kigamboni
Spread the love

TAASISI ya Kinamama na Kinababa kwa Mageuzi ya Jamii (MPFCR), imewataka vijana kuacha matumizi ya mihadarati kutokana na madhara yake. Anaripoti Kamote Martin … (endelea).

Pia imewataka vijana hao kuacha kulalamika kukosa ajira na badala yake watumie fursa zinazowazunguka ili wajipatie kipato.  

Emmy Jahai, Mkurugenzi Mtendaji wa MPFCR ametoa kauli hiyo leo tarehe 4 Oktoba 2019, wakati wa zoezi la usafi na kupanda miti katika Kituo cha Polisi cha Kigamboni.

Amesema, vijana wengi hawajishughulishi na kazi za kuwaingizia kipato na kwamba, wanakaa vijiweni huku wakilalamika kukosa ajira.

Amesema, taasisi yake imekua ikifanya jitihada ya kuwasaidia vijana wenye uraibu wa madawa ya kulevya, ambapo baadhi yao wameacha.

“Zoezi tunalofanya leo ni kufanya usafi, kupanda miti pamoja na kutoa cheti cha heshima kwa mkuu wa kituo hiki cha polisi (ASP Said Msisiri), ikiwa ni kutambua mchango wake wa kuthamini na kujali jamii katika kupambana na vitendo vya uhalifu hapa Kigamboni,” amesema Jahai.

Awali, akisoma risala baada ya zoezi hilo, Dorah Mushi ambaye ni mratibu  wa zoezi hilo amesema, awali kulikua na maeneo mengi hatari kwa watu kutekwa mchana, lakini kwa sasa ulinzi na usalama umeimarishwa.

Ametaja maeneo hayo kuwa ni Midizini, Tungi, Minazi Mikinda, Vijibweni, Feri Bandari, Geza Ulole, Maeneo ya Beach.

ASP Msisiri amesema, Jeshi la Polisi litaendelea kupambana na baadhi ya mawakala wa madawa za kulevya.

Amesema, MPFCR inapaswa kuigwa kwa mchango wake wa kuanzisha kituo cha kuwahudumia watu wenye uraibu wa madawa ya kulevya (Sobber’s House).

Amina Mbonde, mmoja wa waathirika wa madawa ya kulevya ameshauri vijana kuacha matumizi ya dawa hizo kwa kuwa yana madhara mengi ikiwa ni pamoja na matatizo ya akili n ahata kifo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga kuongoza usambazaji wa mitungi ya gesi 10,000 ya Taifa Gas

Spread the loveNaibu Waziri wa Nishati, Judith Kapinga ameahidi kuongoza kwa ufanisi...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wafanyabiashara, wawekezaji China waridhia kuwekeza bil. 800 katika sekta 5 nchini

Spread the loveUJUMBE wa wafanyabiashara na wawekezaji wakubwa kutoka Jimbo la Changzhou...

Habari Mchanganyiko

Bil. 4.42 kumaliza uhaba maji kata 2 Musoma Vijijini

Spread the loveWANANCHI wa kata za Busambara na Kiriba, Jimbo la Musoma...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Soko nepi za watoto lashuka, watu wazima lapaa

Spread the loveKiwanda cha kutengeneza nepi cha Japan kimetangaza kuwa kitaacha kutengeneza...

error: Content is protected !!