Thursday , 25 April 2024
Home Kitengo Michezo Morrison ‘akwea pipa’ kuifuata Kagera
Michezo

Morrison ‘akwea pipa’ kuifuata Kagera

Bernard Morrison
Spread the love

WINGA wa klabu ya Yanga, Bernard Morrison amesafiri kwenda kuungana na kikosi cha Yanga kinachoelekea mkoani Kagera, kuvaana na wenyeji wao Kagera Sugar kwenye mchezo wa Ligi Kuu siku ya Jumatano, kwenye Uwanja wa Kaitaba. Anaripoti Kelvin Mwaipungu, Dar es Salaam … (endelea).

Winga huyo ambaye alisalia Dar es Salaam baada ya kocha wa kikosi hicho, Luc Eymael kusema kuwa hakuwa sehemu ya mpango kwenye mchezo dhidi ya Biashara ambao ulichezwa Mara baada ya kuwa na sintofahamu nyingi licha ya kurejea kwake mazoezini.

Kupitia ukurasa wake kwenye mtandao wa kijamii wa Instagram, mchezaji huyo aliweka picha ikimuonesha yupo kwenye ndege na kuandika ujumbe mfupi wa maandishi kuwa yupo njiani kuelekea Kagera.

Morrison anakwenda kuongezea nguvu kwenye kikosi hicho baada ya kukosekana kwa muda mrefu na kufanya kuwa sehemu ya maandalizi ya kujiandaa na mchezo dhidi ya Simba siku ya Jumapili kwenye hatua ya nusu fainali ya michuano ya Kombe la Shirikisho.

Licha ya kwenda kujiunga na wanzake mchezaji huyo hivi karibuni alikuwa kwenye mgogoro na uongozi wa klabu hiyo kwenye masuala ya mkataba, na baadae kutoroka kambini hatua ambayo ilimfanya kocha wa kikosi hiko kumfukuza kwa sababu za utovu wa nidhamu.

Yanga inakwenda kuvaana na Kagera Sugar ambayo waliondosha kwenye michuano ya kombe la shirikisho kwenye hatua ya robo fainali kwa ushindi wa mabao 2-1.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

EPL, Ligue 1 na Coppa Italia kinawaka leo

Spread the love  LEO ligi kadhaa zitaendelea nchini barani ulaya ikiwemo ligi...

BiasharaMichezo

NBC yaunga mkono jitihada kutokomeza malaria

Spread the loveKuelekea Maadhimisho ya siku ya malaria Duniani yatakayofanyika kesho Aprili...

Michezo

Arsenal dhidi ya Chelsea ngoma nzito leo EPL

Spread the love  Leo kutakua na mchezo mkali sana pale kwenye ligi...

Habari MchanganyikoMichezo

NBC yanogesha Derby Kariakoo, Aziz Ki aibuka mchezaji bora Machi

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambayo ni mdhamini Mkuu...

error: Content is protected !!