Saturday , 20 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Mo aitwa Singida, wazee wataka kufanya yao
Habari MchanganyikoTangulizi

Mo aitwa Singida, wazee wataka kufanya yao

Spread the love

MFANYABIASHARA maarufu Mohammed Dewji ‘Mo’ ameombwa kwenda mkoani Singida ili apozwe machungu. Anaandika Mwandishi Maalum … (endelea).

Akizungumza na wanahabari kwenye viwanja vya CCM Singida baada ya kupatikana Mo, Mzee Juma Mwandoghwe amesema, wazee wanataka kumchinjia mbuzi na kufanya dua kutokana na kutendewa unyama wa kutekwa na watu wasiojulikana.

Mo ni mzaliwa wa Singida ambaye ameongoza jimbo hilo kwa miaka 10 (2005-2015).

Hata hivyo, haijafahamika kama Mo ataitikia wito huo.

Akiwakilisha wazee wenzake, Mzee Mwandoghwe amesema kuwa, Mo anapaswa kutulizwa na kupewa faraja.

Mzee Mwandoghwe amesema kuwa, Mo yupo Dar es Salaam kibiashara na Singida ndio nyumbani hivyo wanao wajibu kwa kijana wao aliyewahi kuwaongoza kwenye jimbo hilo la Singida Mjini.

Mzee Mwandoghwe ameeleza kulaani ukatili alikfanyiwa Mo na kueleza kuwa kitendo hicho ni cha kinyama.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Gardner Habash wa Clouds Fm afariki dunia

Spread the loveALIYEKUWA mtangazaji wa kipindi cha Jahazi kinachorushwa na kituo cha...

Habari za SiasaTangulizi

Rais Samia ataja mikakati ya kufikia trilioni 2 biashara Uturuki, Tz

Spread the loveWakati Tanzania na Uturuki zikidhamiria kuongeza kiwango cha biashara hadi...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wauguzi, madaktari 1000 kugawiwa mitungi ya Oryx Gas

Spread the loveKAMPUNI ya Oryx Gas na Taasisi ya Doris Mollel Foundation...

Habari Mchanganyiko

Tanzania yachaguliwa Makamu wa Rais Tume ya Shirika la Hali ya Hewa Duniani

Spread the love  TANZANIA kupitia Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA)...

error: Content is protected !!