Thursday , 18 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mnapanga kumng’oa Meya Kigoma, thubutuni – Zitto
Habari za Siasa

Mnapanga kumng’oa Meya Kigoma, thubutuni – Zitto

Spread the love

MKAKATI wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), kutumia hila kumng’oa Meya wa Manispaa ya Kigoma, Ujiji, Hussein Ruhava umetua kwa Zitto Kabwe. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Hata hivyo, Zitto ambaye ni mwanasiasa imara wa upinzani na Kiongozi Mkuu wa Chama cha ACT-Wazalendo, amesema ‘thubutuni.’

Jana tarehe 9 Januari 2020, CCM wametangaza kumwondoa Isaya Mwita, aliyekuwa Meya wa Jiji la Dar es Salaam (Chadema), bila kujali kukamilika kwa akidi ya wajumbe wa mkutano uliotumika kumwondoa madarakani.

Mwanasiasa huyo mwenye ushawishi mkubwa wa kisiasa mkoani Kigoma, ametoa onyo hilo tarehe 9 Januari 2020, saa kadhaa baada ya CCM kutangaza kumng’oa Isaya kwa hila.

Zitto ameeleza kuwa, anasubiri kwa hamu watu wanaotaka kumng’oa Meya wa Kigoma, Ujiji anayetokana na chama chake cha ACT-Wazalendo.

Kiongozi huyo wa ACT-Wazalendo ameeleza kuwa, CCM isifikiri Jiji la Dar es Salaam ni sawa na Kigoma.

“Kila nikionana na watu wa CCM, wananiambia Namba 1 kaamua kuwa lazima ushindwe Kigoma Mjini. Hata ukipata kura asilimia 200 hawakutangazi.

“Mimi hucheka na kuwaambia, watu wa Kigoma ni werevu sana. Sasa wanataka kumtoa Meya wa Kigoma, Ujiji kama Dar es Salaam. Watajua Kigoma sio Dar es Salaam. Tunawasubiri,” amesema Zitto.

Amesema, CCM haitafanikiwa kumng’oa Ruhava, kwa kuwa Baraza la Madiwani la Kigoma Ujiji lina madiwani wengi wa ACT-Wazalendo, kuliko wa chama hicho.

Aidha, Zitto amelaani kitendo cha Meya Mwita kuondolewa madarakani, akidai kwamba kitendo hicho ni kinyume na sheria.

“Ninalaani vikali kuondolewa mamlakani kwa Meya wa Jiji la Dar es Salaam, Isaya Mwita kinyume cha Sheria na Kanuni za Serikali za Mitaa. Ninatuma salamu za mshikamano kwa Mwenyekiti wa Chadema,” amesema Zitto.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Tume huru ya uchaguzi yatangaza ajira watendaji daftari wapiga kura

Spread the love  TUME Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC), imetangaza nafasi...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema yatangaza ruti awamu ya pili maandamano

Spread the love  CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimesema awamu ya...

Habari za Siasa

CCM yamkana mwenyekiti UVCCM aliyetaka wapinzani wapotezwe

Spread the love  CHAMA Cha Mapinduzi (CCM), kimejitenga na kauli ya mwenyekiti...

Habari za SiasaTangulizi

Rais Samia kutunukiwa udaktari wa heshima Uturuki

Spread the loveBaraza la Chuo Kikuu cha Ankara, ambacho ni cha pili...

error: Content is protected !!