Thursday , 25 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mlipuko mpya corona, Uingereza yatengwa
Habari za Siasa

Mlipuko mpya corona, Uingereza yatengwa

Spread the love

NCHI ya Uingereza imetengwa na mataifa kadhaa ya Ulaya na Amerika kutokana na mlipuko mpya wa virusi vya corona. Inaripoti mitandao ya kimataifa…(endelea).

Mataifa hayo yakiwemo Argentina, Chile, Colombia na Canada, yamezuia abiria na treni zinazotoka Uingereza kuingia kwenye mataifa yao kuhofia maambukizi mapya kwenye mataifa yao.

Uamuzi wa mataifa hayo ulifikiwa saa chache baada ya Boris Johnson, Waziri Mkuu wa Uingereza kupiga marufuku mikusanyiko kwenye sherehe za Krismas Ijumaa wiki hii.

Waziri huyo amewaeleza Waingereza kwamba, sasa hawana budi kuhakikisha wanafuata kikamilifu taratibu za kujikinga dhidi ya maambukizi ya virusi vya corona.

Mataifa ya France, Ujerumani, Uholanzi, Italia, Ubelgiji, Australia, Ireland and Bulgaria ndio yaliyotangulia kupiga marufuku wageni kutoka Uingereza.

Tayari Waziri wa Afya wa Uingereza, Matt Hancock jana tarehe 20 Desemba 2020, alitangaza sheria kali ili kukabiliana na maambukizi hayo mapya.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

error: Content is protected !!