Wednesday , 24 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Mlimani City watoa sababu za kufungia Nakumatt
Habari MchanganyikoTangulizi

Mlimani City watoa sababu za kufungia Nakumatt

Milango ya duka la Nakumatt likiwa imefungwa
Spread the love

DUKA kubwa (Supermarket) la Nakumatt lililopo jijini Dar es salaam, limelifungia, baada ya kukosa bidhaa za kutosha kwa muda mrefu pamoja na kudaiwa kodi za huduma mbalimbali, anaandika Angel Willium.

Meneja Mkuu wa Mlimani City, Pastory Mroso ameuambia MwanaHALISI Online, kuwa wamechukua uamuzi huo baada ya duka hilo kushindwa kutimiza vigezo walivyowekea ikiwa pamoja na kupewa notisi miezi minne kufanyia marekebisho tatizo hilo.

Mroso amesema pamoja na kuwapa notisi hiyo lakini hakuna hatua yoyote iliyochukuliwa, wakawaongezea tena notisi ya mwisho ya siku kumi ambayo ilikuwa inaisha siku ya Jumamosi, na kuamua kuwafungia asubuhi ya leo.

Meneja huyo ameendelea kwa kusema kwamba tatizo hilo limekuwa likiwaathiri wafanyakazi na hata bidhaa za wafanyabiashara wengine na wamelishalitolea taarifa serikalini kwa hatua zingine zaidi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Bodaboda waeleza mafanikio mafunzo usalama barabarani

Spread the loveMADEREVA bodaboda katika Jiji la Dodoma wameeleza jinsi mafunzo ya...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NBC yaahidi kuendelea kuunga mkono Serikali za Mitaa

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) imesisitiza dhamira yake ya...

Habari Mchanganyiko

Watuhumiwa 12 wa kilo 726.2 za dawa za kulevya wafikishwa mahakamani

Spread the love  WATUHUMIWA watatu wamefikishwa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kibaha Mkoani...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

error: Content is protected !!