MKAKATI wa muda mrefu unaoondeshwa na wabunge pia madiwani kutoka Chama Cha Mapinduzi (CCM), kumng’oa Meya wa Manispaa ya Iringa, sasa umeshika kasi. Anaripoti Mwandishi Wetu, Iringa…(endelea).
Tayari madiwani hao wamepokea wito wa kuhudhuria kikao kilichoitishwa kwa haraka na Hamidu Njovu, Mkurugenzi wa Manispaa ya Iringa. Kikao hicho kimechopangwa kufanyika kesho tarehe 26 Machi 2020 katika ukumbi wa mikutano wa manispaa hiyo.
“Napenda kuwaarifu kuwa mkutano wa baraza maalum la madiwani litafanyika tarehe 26 .03.2020 siku ya Alhamis kuanzia saa 02:00 asubuhi…,” umeeleza wito huo na kuongeza:
“Kwa barua hii mnaalikwa rasmi kuhudhuria mkutano huo bila kukosa…”
Mkakati wa wabunge wa CCM Iringa kupanga njama za kumng’oa Alex Kimbe, Meya wa Manispaa ya Iringa ulishika kasi baada ya Isaya Mwita, Meya wa Jiji la Dar es Salaam kumkaba koo wakitaka kumtimua. Isaya aligoma baada ya taatibu kushindwa kukamilika
Meya Kimbe (Chadema), alianza kusakamwa na baadaye kupewa barua ya kujieleza kutokana na kuvishwa tuhuma nne.
Tuhuma hizo ni ukosefu wa adabu, matumizi mabaya ya madaraka, matumizi mabaya ya rasilimali za halmashauri na vitendo vya rushwa.
Tarehe 2 Machi 2020, Meya Kimbe alisema amepokea barua iliyobeba tuhuma hizo za kupikwa kwa sababu maalum za kisiasa.
“Nitapeleka barua kwa mkurugenzi wa manispaa ili nimweleze na kumkumbusha vyombo vya usalama na watendaji wake taratibu na kanuni za kumtoa Meya madarakani wamezikosea,” alisema.
Meya Kimbe alisema, CCM, kimekosa fursa kwa wananchi na sasa kinatumia hila kukabili maeneo yanayoongozwa na wapinzani ikiwemo Manispaa ya Iringa.
Leave a comment